Facebook Comments Box

Monday, October 13, 2014

TETESI ZA KUCHINJWA WATOTO TABATA: WAZAZI WAKUSANYIKA SHULE YA MSINGI TABATA

Kutokana na tetesi za kuwa watoto watatu wa shule ya msingi tabata kutekwa na kuchinjwa wazazi wamekusanyika katika shule ya msingi tabata. Katika eneo hilo kuna shule za msingi tatu zilizopo pamoja.

Wazazi wamejaa hapo baada ya kupata taarifa kuwa gari aina ya Noah ambayo inatumika kuwakamata watoto imeshikwa na walimu na ipo hapo shuleni.

Kuna baadhi ya wazazi wanawataka watoto wao warudi nao nyumbani. Ni muda sasa kumekuwa na tetesi za watoto kushikwa na kuchinjwa na Noah yenye vioo vyeusi. Kwa leo wazazi wamekusanyika baada ya uvumi kuzagaa kuwa watoto watatu walio kamatwa na Noah hiyo wamechinjwa.


Kitongoni blog wakati inafika eneo la shule ilikuwepo noah ambayo ni nyeusi ya mmoja wa walimu na huja nayo shuleni hapo kila siku za kazi. Mwalimu mkuu ameahidi kutoa maelezo kwa wazazi baadae.

Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU