Facebook Comments Box

Tuesday, October 14, 2014

KANISA KATOLIKI LAJADILI KUHUSU WAPENZI WA JINSIA MOJA

Makasisi wanaoshiriki katika mkutano wa maaskofu wanaangazia masuala ya mafunzo ya kanisa katoliki kwa familia ,wametoa mwito kwa kanisa hilo duniani kuwachukulia watu wenye mapenzi ya jinsia moja kwa usawa 

Kauli hii inakuja baada ya Maaskofu kuandika ripoti wakati wa mkutano wa synodi ukiendelea huko Vatican na kusema kuwa wapenzi wa jinsia moja wana zawadi na viwango vya kutoa kwenye jumuiya za kikristo hii ikiwa ni ripoti iliyotolewa mapema wiki hii.

Ripoti hiyo haitoi changamoto yoyote kwa msimamo wa muda mrefu wa kanisa hilo juu ya kupinga ndoa za jinsia moja,lakini baadhi ya vikundi vya kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja wanachukulia kauli hiyo kuwa ya mafanikio makubwa kwa jamii zao.

Na moja ya makundi yenye kushikilia msimamo mkali kikanisa wametupilia mbali ripoti hiyo na kuuita ya kisaliti.

Zaidi ya maaskofu 200 wa kanisa katoliki wanakutana kwenye mkutano wa synodi tangu mapema mwezi huu,katika mkutano huo ni papa Francis aliyetoa mwito wa kujadili masuala ya utoaji wa mimba,vidonge vya uzazi wa mpango,mapenzi ya jinsia moja na talaka.

Papa Francis amewataka viongozi wa juu wa kanisa hilo kuzingatia Zaidi suala la wapenzi wa jinsia moja chanya kuliko kuwa kinza na amefanikiwa kuwateka maaskofu wanaohudhuria mkutano huo wa sinodi.

Mwaka uliopita katika ripoti aliyo itoa papa Francis kuhusiana na mwenendo wa kanisa katoliki kuwa waumini walio wengi waliliacha mkono kanisa hilo kutokana na mafunzo yahusianayo na ngono na dawa za uzazi wa mpango.

Papa huyo anazichukulia ndoa hizo za jinsia moja kama zisizo na utaratibu akiinukuu ripoti ya kanisa katoliki iliyochapishwa mwaka 1986,wakati Papa Francis alipokua mshauri mkuu wa masuala ya teolojia ya kanisa katoliki wa hayati papa John Paul wa pili.

Nguvu kubwa ya vikundi vya kutetea haki za watu wenye mapenzi ya jinsia moja ni juu ya kauli ya papa Francia aliyoitoa mwishoni mwa mwaka wa jana alipokuwa kwenye kambi ya vijana wa kanisa hilo huko Rio de Jeneiro alitoa kauli kua kama mtu anamtafuta Mungu na ana nia njema ,yeye ni nani wa kuhoji?

Papa Francis anaingia katika historia ya kanisa katoliki ulimwenguni kutumia jina (hasha kum si matusi) WASENGE hadharani kuliko kutumia neno wapenzi wa jinsia moja.

CHANZO: BBC SWAHILI


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU