Facebook Comments Box

Thursday, October 16, 2014

SIMBA NA YANGA NA IMANI ZA USHIRIKINA WA MVUA

 KIKOSI CHA TIMU YA SIMBA.
 WACHEZAJI WA SIMBA WAKIMSIKILIZA KOCHA WAO PATRICK PHIRI.
 KIKOSI CHA TIMU YA YANGA.
WACHEZAJI WA YANGA WAKISHANGILIA MOJA YA BAO LAO.
kitongoni blog:


Mpaka  kwenye  miaka  ya  90  kulekea  mpambano  wa  watani  wa  jadi  kulikuwa  na  imani  za  kishirikiana za mvua  zikichukua  nafasi  kuliko  hivi  sasa, itakumbumbukwa  kwamba  ilifikia  hatua  timu  ya  Yanga  wanapoona  mvua  imenyesha  wao  walikuwa  wakiingiwa  na  hofu  zaidi  ya  kuupoteza mchezo  huo  huku  upande  wa  pili  wa  Simba nao  wakichekelea  kunyesha  kwa  mvua   wakimaanisha  kuwa  lazima  wataibuka  washindi.

Ama  kwa  hakika  tukio hilo  lilikuwa  lina  nafasi  kubwa  kwa  kuwa  kweli  siku  ya  mpambano  huo  kama  mvua  haikunyesha  Simba  walifungwa  au  kutoka  sare  na  pale  iliponyesha  mvua  tu  ni  lazima  Yanga  wangefungwa.

Lakini  kunako  miaka  hii  ya  2000  mambo   sasa  yamebadilika  na  yeyeto  Yule  anaweza  kupata  ushindi  katika  hali  yoyote  ile liwake  jua  ainyeshe  mvua,  na  hili  ndiyo  miongoni  mwa  mambo  yanayozidi  kuupa  ladha  mchezo  huu  kuwa  vigumu  kupata  utabiri  wa  nani  mshindi. 

Jambo lingine  ni  zile  kambi  zao  ambazo  kama  Yanga  wakitokea  Pemba  au  Bagamoyo   Mbegani  huwa  wana  uhakika  zaidi  wa  kupata    ushindi  kuliko   kuweka  kambi  yao  Jijini  Dar  es  salaam,  wakati  Simba  wao  huwa  wana  uhakika  zaidi  wa  kupata  ushindi  kama  tu  wametokea  Unguja  au  Dar  es  salaam  maeneo  ya  Bamba  Beach. 

Katika  mechi  hii  kambi  za  timu  zote  hizo  hazikuwa  kwenye  sehemu  zile  zilizo zoeleka  na hali  hiyo  imefanya  kuwa  na  tambo  nyingi  kutoka  kwa  mashabiki  wake  na kila  upande  kuamini  kuwa  wataibuka  washindi.

Jicho  la  kitongoni blog litakuwepo  kukujuza  kila  kitu  ambacho  kitatokea  ikiwa  ni  pamoja  na  visa na  vibweka  vyote  vitakavyojiri  uwanja  wa  Taifa  tarehe  18/10/2014, Jumamosi.




 



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU