Facebook Comments Box

Friday, September 5, 2014

JOAN RIVERS AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu nchini Marekani Joan Rivers amefariki dunia akiwa na umri wa miaka themanini na mmoja.

Joan alikua amelazwa katika hospitali moja mjini New York kwa wiki kadhaa sasa akisumbuliwa na maradhi ya moyo. Melissa binti wa Joan, Akitangaza juu ya kifo cha mamake alimuelezea mama yake kuwa maishani mwake alikua akipenda kuona watu wana tabasamu usoni ama vicheko.

Joan River alianza shughuli zake za ucheshi kama muigizaji wa kawaida tu nusu karne iliyopita, na anatajwa kuwa mwanamke maarufu na bora katika ucheshi jukwaani.

CHANZO: BBC SWAHILI


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU