Facebook Comments Box

Thursday, August 14, 2014

ANGALIA JINSI KIBONDE NA GARNER WALIVYO FIKISHWA MAHAKAMANI

Watangazaji Ephraim Kibonde (wa kwanza kushoto) na
mwenzake Gardner Habash (wa pili kulia) wakielekea
kizimbani.

Watangazaji hao wakiongozwa na maofisa wa polisi
kuelekea mahakamani.

...Wakiingia mahakamani.

MTANGAZAJI wa Clouds FM, Ephraim Kibonde na
mwenzake, Gardner Habash wa Times FM leo
wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya
Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa kusababisha ajali na
kudharau amri ya polisi na kutoa lugha ya matusi.
Watangazaji hao wamesomewa mashitaka hayo na Wakili
wa Serikali, Salim Mohammed mbele ya Hakimu Aniseta
Wambura.
Kibonde na Gadna wanadaiwa kutenda makosa hayo
Jumamosi ya Agosti 9, mwaka huu saa 12 asubuhi, katika
eneo la Makumbusho, ambapo Kibonde akiwa anaendesha
gari walilokuwa wamepanda aliligonga gari la raia mmoja
wa kigeni (Mzungu) na kukimbia.
Kesi yao imeahirishwa mpaka Septemba 10 mwaka huu
itakaposikilizwa tena.(Picha na Shakoor Jongo / GPL)


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU