Facebook Comments Box

Tuesday, June 10, 2014

SHEIKH MWINGINE AUAWA KWA KUPIGWA RISASI KENYA

Mwenyekiti wa Baraza la maimamu nchini Kenya auawa kwa
risasi Mwenyekiti wa baraza la maimam na muhubiri maarufu nchini Kenya Sheikh Mohammed Idris, ameuawa kwa kupigwa risasi mjini Mombasa.

Sheikh Mohammed Idris ameuawa karibu na msikiti ulio karibu na
nyumbani kwake eneo la Likon baada ya kuvamiwa na watu waliokuwa na silaha, wakati akitoka nyumbani kuelekea msikitini.

Taarifa kutoka katika eneo hilo zinasema kuwa Sheikh Mohammed
Idris alikuwa akipata vitisho vya mara kwa mara na amewahi kutoa taarifa za vitisho hivyo na kusema kuwa anahofia maisha yake.
Mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya kumbukumbu ya Pandya, mjini Mombasa. Pamekuwa na matukio ya mara kwa mara ya mauaji ya viongozi maarufu wa dini nchi kenya katika mazingira ya kutatanisha.
Inna lilahi wa inna ilayhi rajiiun.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU