Facebook Comments Box

Sunday, September 1, 2013

JESHI LA POLISI LATOA TAMKO KALI KWA WAPIGA PICHA ZA UTUPU


Jeshi la Polisi Kanda ya Kinondoni limetoa kauri nzito kuhusu picha za udhalilishaji zilinazosambazwa na wasanii  na baadhi ya watu hapa nchini..

Akiongea katika mahojiano maarumu mkuu wa kituo cha Polisi Oysterbay “OCD” Mtafungwa alisema kuwa kimsingi kupiga picha za utupu ni kosa kisheria hivyo endapo muhusika akimatwa atashtakiwa kwa mujibu wa sheria.

Mtafungwa aliendelea kufafanua na kusema kuwa "Jeshi la Polisi lipo kwa ajili ya kusimamia sheria iliyowekwa na serikali hivyo huwa kuna namna ya kuwakamata wahusika hasa kama kumetokea malalamiko toka idara flani kuhusiana na matukio yoyote yanayopelekea uvunjifu wa amani au kupotosha maadili” Alisema Kamanda huyo kipenzi cha watu

Aidha Kamanda huyo aliendelea kufafanua “ Pia Jeshi la polisi linamamlaka ya kumkamata mharifu yeyote kwa muda wowote endapo kipindi hicho akikutwa anafanya uharifu ni pamoja na upigaji picha hizo chafu, Lakini kubwa tuhajitaji kumkata mtu na ushahidi ili iwe rahisi kumbana na kumfikisha mbele ya sheria” Alisema

Mtafungwa alimaliza kusema Pindi tupatapo taarifa kuhusuiana na picha hizo chafu “ Tutaendelea kufatilia kupita mitandao ya kijamii ili kuona hizo picha zikoje halafu kuwatolea taarifa hadharani kupita kwa msemaji wa Jeshi la Polisi Kanda ya Kinondoni RPC Wambura ambae kisheria ndiye mwenye mamlaka ya kusema” 
na kumchukulia hatua kali mpigaji wa picha hizo.
Alisema Mtafungwa


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU