Facebook Comments Box

Wednesday, February 13, 2013

TANZIA: SHEIKH NASSOR ABDALLAH BACHOO

UPDATE/TAARIFA MPYA

Waheshima  Taarifa Kamili ya Maziko ya Mpendwa Shekh wetu Nassor Bachu yatafanyika Kesho katika Msikiti wa Kikwajuni Saanne Asubuhi

Kwa taarifa ya jamaa wa marehemu waliitowa marehema amefarikia majira ya saa nne asubuhi ya yale, baada ya kuuguwa kwa muda mrefu,  marehemu alisafirisha Mjini Dar-es-Salaam kwa matibabu zaidi.kwa kipindi alikuwa akipata matibabu katika hospitali za Mjini Dar. hatima marehemu  amerejeshwa Zanzibar na kuendelea na matibabu.

Shekh. Nassor alikuwa akipata matibabu kwa jamaa zake nje kidogo ya mji wa Zanzibar katika maeneo ya Chukwani hadi mauti yanamkuta leo asubuhi alikuwa chukwani Zanzibar.

 Maziko yatafanyika kesho katika msikiti wa Kikwajuni na kuzikwa Kijijini kwao Donge Mkoa wa Kaskazini Unguja, Zanzibar.

Mwenyezi Mungu amlaze pema peponi

Innaa lillahi wainnaa ilayhi raajiuun.

Sheikh Nassor Abdalla Bachoo ametangulia mbele ya haki.

Allahumma thaabit-hu biqauli thaabit. Allahumma gh-firlahu warhamhu waafihi waaf-anhu.

Sheikh Nassor Abdalla Bachoo hatosahaulika kamwe kwa mchango wake mkubwa katika elimu ya Uislamu na maendeleo ya Uislamu kwa ujumla ndani ya Afrika Mashariki na ulimwengu kwa jumla.

Kwa niaba ya Familia yangu natanguliza mkono wa ta’azia kwa familia ya sheikh, ndugu, jamaa na Waislamu wote kwa kuondokewa na kiungo muhimu katika dini yetu tukufu ya Kiislamu.

Tunamuomba Allah Taala kwa utukufu Wake Ampokee sheikh miongoni mwa waja wake wema, Amsamehe madhambi yake na Amjazie penye upungufu. Ameen.

Tembelea bog: Miujiza-ya-quran na/au Facebook: Groups/Miujiza ya Quran
Kama kutakuwa na maswali tafadhali usisite kuwasiliana kwa email: miujizayaquran@gmail.com

Shukran

kitongoni.blogspot.com inaungana kuwaombeeni faraja nyote mlioguswa na msiba huu. Roho ya marehemu Sheikh Nassor Abdalla Bachoo ipumzike pema! AMIN!



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU