Facebook Comments Box

Saturday, November 23, 2013

ZITTO KABWE KUONGEA NA WAANDISHI WA HABARI KESHO

Bila shaka hili ni jambo ambalo mimi na wewe tulilitarajia. Baada ya maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA ya kuwavua madaraka ya kiuongozi waliyokuwa nayo Mh.Zitto Kabwe na Dr.Kitila Mkumbo hapo jana, wawili hao wapo tayari kukutana na waandishi wa habari na kuueleza umma maoni na msimamo wao.
Katika ujumbe mfupi ambao Mh.Zitto Kabwe ameuweka kwenye ukurasa wake wa Facebook na taarifa hiyo hiyo kusambazwa kwa vyombo mbalimbali vya habari, mkutano na waandishi wa habari unatarajiwa kufanyika hapo kesho saa tano [asubuhi] katika Hoteli Ya Serena jijini Dar-es-salaam.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU