Facebook Comments Box

Friday, November 22, 2013

TETESI: MAKAMU MWENYEKITI WA CHADEMA AJIUZULU RASMI NA YEYE

Saidi arfi - makamu mwenyekiti wa chadema ajiuzulu rasmi

Saidi Arfi - Makamu Mwenyekiti wa chadema ajiuzulu rasmi nafasi yake jioni hii.

Arfi ambaye pia ni mbunge wa Mpanda mjini (CHADEMA) amefikia uamuzi huo leo baada ya kile kilichofanywa na kamati kuu ya CHADEMA kuwavua uongozi Zitto Kabwe na Dr. Kitila Mkumbo.

Nafasi ya Zitto amepewa mchungaji Peter Msigwa

CHINI NI BARUA PEPE INAYO DAIWA KUTUMWA NA MBUNGE HUYO KWA CHAMA

From: Said Amour Arfi <said_arfi@yahoo.com>
Date: November 22, 2013 3:45:47 PM GMT+03:00
To: "mbowe2008@gmail.com" <mbowe2008@gmail.com>
Cc: "slaa@chadema.or.tz. zittokabwe@gmail.com" <slaa@chadema.or.tz. zittokabwe@gmail.com>

Subject: KUJIUZULU MAKAMU MWENYEKITI (BARA)

Salaam,

Napenda kuwasilisha kwako taarifa ya kujiuzulu nafasi ya Makamu Mwenyekiti Bara kuanzia Leo Ijumaa 22 Novemba 2013 kwa kuchoshwa na Unafiki unaoendelea ndani ya Chama. Napenda ifahamike pia kwangu maslahi ya Wapiga kura, Wakaazi na wananchi wa Mpanda Mjini na Wilaya ya Mpanda ni muhimu katika kuwatumikia, hivyo basi sipo tayari kuchaguliwa marafiki.

Kwa kipindi kirefu zimekuwepo shutma dhidi yangu na kutiliwa mashaka mahusiano yangu na Mhe Pinda Waziri Mkuu pamoja na kulijadili katika vikao kadha Mpanda na Dar es Salaam bado yapo mashaka kwa nini alipita bila kupingwa hayo yalikua maamuzi ya Wanampanda kwenu imekua ni tatizo lakin hamsemi kwa nini Majimbo mengine 16 nchini yalipita bila kupingwa mlikua wapi na nani alaaumiwe huu ni Unafiki wa kupindukia.

Aidha mmechukizwa sana kwa nini nilihoji kauli ya Muasisi wa Chama Mhe Mtei kutuchagulia viongozi naomba ifahamike wazi kwamba huu ni mtazamo wangu na utabakia hivyo siku zote kwa chama cha demokrasia kutoruhusu uongozi wa kiimla kwa kukidhi matakwa ya Waasisi ambao huvigeuza vyama kuwa Mali binafsi

Kwa kusema ukweli na kusimamia ukweli daima itabakia kuwa lengo langu katika maisha yangu siku zote hata kama itanigharimu maisha yangu

Nawasilisha.

Said A Arfi (mb)



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU