Facebook Comments Box

Saturday, August 24, 2013

YANGA WAIKARIBISHA ASHANTI KWENYE LIGI KUU KWA KIPIGO CHA MBWA MWIZI

Kikosi cha Yanga

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yana SC wameanza vema kampeni za kutetea taji lao, baada ya kuwafumua Ashanti United ‘Watoto wa Jiji’ mabao 5-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mabao ya Yanga leo yalifungwa na Jerry Tegete dakika za 10 na 57, Simon Msuva dakika ya 47, Haruna Niyonzima dakika ya 73 na Nizar Khalfan dakika ya 90, wakati bao pekee la Ashanti lilifungwa na Shaaban Juma dakika ya 89
Young Africans inayonolewa na kocha mholanzi Ernie Brandts imeanza vizuri harakati zake za kutetea Ubingwa kwa kuhakikisha inashinda mchezo wa mwanzo na ndivyo vijana wa Jangwani walivyofanya.
Ilimchukua dakika 10 Jerson Tegete kuipatia Young Africans la kwanza kwa kumchambua mlinda lango wa Ashanti kufuatia pasi nzuri wa winga wa kulia Saimon Msuva kuitoka ngome ya Ashanti na kumpasia mfungaji aliyeukwamisha mpira wavuni bila ajizi. 
Ashanti walifanya mashambulizi langoni mwa Yanga kupitia kwa Hussein Sued lakini ukuta wa Yanga uliokuwa chini ya Mbuyu Twite na nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro' ulikuwa kikwazo kwake kumfikia mlinda mlango Ally Mustapha 'Barthez'.
Kiungo Athuman Idd 'Chuji' alitolewa nje dakika ya 18 ya mchezo kuufuaia kuumia na kushinda na kuendelea na mchezo na nafasi yake kuchukuliwa na kiungo Frank Domayo 'Chumvi' . 
Kutokua makini kwa washambuliji wa Yanga Didier Kavumbagu, Saimon Msuva na Jerson Tegete kulizifanya timu kwenda mapumziko zikwa 1-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Yanga kujipatia bao la pili dakika ya 48 ya mchezo kupitia kwa mshambuliaji Saimon Msuva aliyewatoka walinzi wa Ashanti na kuachia shuti kali liliokwenda moja kwa moja wavuni.
Jerson Tegete aliipatia Young Africans bao tatu dakika ya 58 kwa usatdi wa hali ya juu akimalizia pasi safi ya Saimon Msubva aliyewatoka walinzi wa Ashanti United na kujaza krosi safi ambayo Tegete aliiweka kifuani kabla ya kumchambua mlinda mlango.
Yanga iliendelea kucheza inavyotaka huku ikitawala dimba la katikati kupitia kwa viungo wake Haruna Niyonzima, Salum Telela na Frank Domayo hali iliyowapelekea wachezaji wa Ashanti kucheza faulo nyingi na mwamuzi kuwaadhibu kwa kadi za njano na mmoja wao kutolewa nje kwa kadi nyekundu.
Haruna Niyonzima aliipatia Young Africans bao la nne dakika ya 74 ya mchezo kwa kichwa, akimalizia mpira wa adhabu uliopigwa na mlinzi wa pembeni David Luhende kufuatia Saimon Msuva aliyekuwa amechezewa madhambi na walinzi wa Ashanti United.
Dakika ya 90 Ashanti United walijipatia bao kupitia kwa Shaban Juma kufuatia uzembe wa walinzi wa Yanga waliotegeana kumkaba mfungaji aliyeukokota mpira toka nje ya 18 na kuingia nao ndani ya sita na kumfunga mlinda mlango Ally Mustapha 'Barthez'.
Huku washabiki na wapenzi wa soka wakiwa wanatoka nje wakijua mpira umemalizika, Nizar Khalfani aliipatia Young Africans bao la tano na kukamilisha ushindi huo mnono akimalizia pasi ya Saimon Msuva ambaye leo alikua mwiba mkali kwa walinzi wa Ashanti.
Mpaka dakika 90 za mchezo za mwamuzi Israel Mjuni Nkongo zinamalizika, Young Africans 5 -1 Coastal Union.
Kocha mkuu wa Yanga Ernie Brandts amekipongeza kikosi chake na kusema ni mwanzo mzuri katika msimu huu, aidha amesema wachezaji wake wangekuwa makini basi leo wangeibuka na ushindi mnono zaidi ya hizo bao tano walizozipata kutoka kwa wauza mitumba wa Ilala - Ashanti united.
Mara baada ya mchezo wa leo wachezaji wote wamepewa mapumziko siku ya kesho mpaka siku ya jumatatu watakapoanza mazoezi kujiandaa na mchezo dhidi ya Coastal Union ya Tanga siku ya jumatano tarehe 28.08.2013 katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Young Africans: 1.Ally Mustapha 'Barthez', 2.Juma Abdul, 3.David Luhende, 4.Nadir Haroub 'Cannavaro', 5.Kelvin Yondani, 6.Athuman Idd 'Chuji'/Frank Domayo, 7.Saimon Msuva, 8.Salum Telela, 9.Didier Kavumbagu/Hussein Javu, 10.Jerson Tegete/Nizar Khalfani, 11.Haruna Niyonzima


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU