Facebook Comments Box

Tuesday, August 6, 2013

POLISI, RAIA 2 JELA MIAKA 7 KWA KUIBA MILIONI 33O ZA JESHI LA POLISI

WATU watatu akiwemo aliyekuwa Polisi, Edna Kadogo wamehukumumiwa kifungo cha miaka saba jela katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam baada ya kupatikana na hatia ya kula njama na kuiba Sh milioni 330 mali ya Jeshi la Polisi.

Hakimu Gene Dudu alitoa hukumu hiyo baada ya kuridhika na ushahidi pamoja na vielelezo vilivyowasilishwa na upande wa mashitaka.

Washitakiwa hao walikuwa wanakabiliwa na mashitaka matatu ya kula njama, kughushi na wizi wa kiasi hicho cha fedha kwenye akaunti namba 2011000015 inayoitwa Police Retention Collection kwenye benki ya NMB Meatu.

Akisoma hukumu hiyo , Hakimu Dudu alisema upande wa mashitaka umethibitisha bila kuacha shaka mashitaka mawili dhidi ya washitakiwa watatu na mahakama imewaona wana hatia.

Alisema katika mashitaka ya kula njama watatumikia kifungo cha miaka miwili jela na wizi wa Sh milioni 330 watatumikia kifungo cha miaka mitano jela.

Adhabu hizo zitakwenda pamoja ambayo ni sawa na kifungo cha miaka mitano. Mbali na Kadogo, washitakiwa wengine waliotiwa hatiani ni mfanyabiashara Joshua Aseno na Mfanyakazi wa Benki, Adelina Lwekoramu.

Baada ya kutoa hukumu hiyo, Hakimu Dudu alimuaru, Aseno arudishe Sh milioni 30 na nyingine zilizoingizwa kwenye akaunti yake kutoka katika akaunti ya polisi na Kadogo anatakiwa kurudishwa milioni 10.

Aidha mahakama imewaachia huru washitakiwa Vedastus Mafuru, Kennedy Achayo, Luciana Limbu, Agnes Maro, Mkika Nyasebwa, Amos Hangaya. kwa kuwa upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yao.

Kesi hiyo ilikuwa ikikabili washitakiwa 11 lakini Fortunatus Biseko na Deogratias Lumato waliachiwa huru baada ya kuonekana hawana kesi ya kujibu na hivyo wakabaki tisa

Source: WAVUTI


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU