Facebook Comments Box

Thursday, August 15, 2013

MKURUGENZI WA CRDB KORTINI KWA TUHUMA ZA KUDHALILISHA KIJINSIA

Mkurugenzi wa Benki ya CRDB tawi la Moshi mkoani Kilimanjaro, Francis Mollel jana alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi kwa tuhuma za kumdhalilisha kijinsia mteja ndani ya benki hiyo, Lulu Kajembe.

Mwendesha mashitaka, wakili wa serikali, Patrick Mwita mbele ya Hakimu Swai alieleza kwamba Lulu aliwahi kufanya kazi kwenye benki hiyo na kwamba siku ya tukio Juni 1, 2013, mlalamikaji alikuwa kwenye foleni akisubiri kuhudumiwa ndani ya benki hiyo na ndipo mshitakiwa alimtolea maneno ya udhalilishaji wa kijinsia.

Hata hivyo, mshitakiwa anayetetewa na wakili Kitomo, alikana kosa na mahakama hiyo kumpa dhamana ya shilingi milioni moja na wadhamini wawili wanaotambulika. Mshitakiwa yupo nje kwa dhamana ambapo amezuiwa kusafiri nje ya mkoa na kuwasilisha stakabadhi zote za kusafiria.

Kesi hiyo iliahirishwa hadi Agosti 21 itakapotajwa. --- (TANZANIA DAIMA)


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU