Facebook Comments Box

Friday, July 26, 2013

UBALOZI WA MAREKANI WAIPONGEZA TTCL KWA KUTOA HUDUMA BORA ZA MAWASILIANO


US1Kiongozi wa ujumbe kutoka ubalozi wa Marekani hapa nchini Bw.Jeff Shrader akitoa shukrani zake kwa uongozi na wafanyakazi wa TTCL alipotembelea makao makuu ya Kampuni hiyo.US11Afisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa TTCL Bw. Peter Ngota akiwashukuru wawakilishi kutoka ubalozi wa Marekani hapa nchini kwa kutambua mchango wa         TTCL katika kufanikisha ziara ya Rais wa Marekani alipotembelea Nchini Tanzania.
US14
Uongozi wa TTCL pamoja na wawakilishi wa Ubalozi wa Marekani hapa nchini katika picha ya pamoja.
 
 Afisa Mtendaji mkuu wa TTCL Dtk. Kamugisha Kazaura akibadilishana mawazo na Kiongozi wa ujumbe kutoka ubalozi wa Marekani hapa nchini Bw. Jeff Shrader.US16Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa Kiongozi wa ujumbe kutoka ubalozi wa Marekani hapa nchini Bw. Jeff Shrader.
Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) imepongezwa na Ubalozi wa Marekani kwa huduma bora iliyotoa  wakati wa ujio wa Rais wa Marekani hapa nchini.
Akitoa shukrani hizo Kiongozi wa ujumbe kutoka  ubalozi wa Marekani hapa nchini Bw. Jeff Shrader amesema, Ubalozi wa Marekani Nchini Tanzania umejipatia sifa kubwa kwa huduma bora na za uhakika  kutoka TTCL wakati wote wa ujio na uwepo wa Rais wa Marekeni hapa nchini.
Ameongeza kuwa huduma walizozipata  zimethibitishwa na taarifa kutoka ofisi inayoratibu safari za Rais wa Marekani kuwa katika nchi walizopita Afrika huduma ya mawasiliano ialiyoipata Tanzania ilikuwa ni ya kiwango cha juu na aliipongeza TTCL na kusema hii ni sifa kubwa kwa Serikali ya Tanzania na Ubalozi wa Marekani hapa nchini.
Katika Shukurani zake Bw. Jeff Shrader alioa pia zawadi kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura  na kwa baadhi ya wawakilishi kutoa fani mbalimbali za Ufundi na Biashara kwa niaba ya wafanyakazi wote wa TTCL kama ishara yao ya shukurani kwa TTCL na Taifa kwa ujumla.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU