Facebook Comments Box

Wednesday, July 17, 2013

PICHA: MAJENGO YA SCHOOL OF LAW YAKABIDHIWA KWA SERIKALI

Picture
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bibi Christina Sonyi akitia saini hati ya makabidhiano ya majengo ya Law School of Tanzania wakati wa shughuli ya makabidhiano ya majengo hayo iliyofanyika jana Julai 16,2013 jijini Dar Es Salaam. Wanaoshuhudia ni Bw. Emmanuel Mayeji kutoka Wizara ya Katiba na Sheria (wa kwanza kulia), Mh. Jaji Gerald Ndika Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (wa pili kulia), na wa kwanza kushoto ni Bw. Aloyse P. Mushi Mkurugenzi Mtendaji kutoka Co-architecture.
Picture
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bibi Christina Sonyi amepokea hati ya makabidhiano pamoja na funguo za majengo ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo kutoka kwa Naibu Meneja wa Kampuni ya Beijing Construction Engineering Group, Bw. Zhang Chengwei iliyokuwa ikijenga majengo hayo na kukamikika.

Makabidhiano hayo yalifanyika jana, siku ya Jumanne, Julai 16, 2013 jijini Dar es Salaam.

Anayeshuhudia katikati ni Bw. Aloyse P. Mushi, Mkurugenzi Mtendaji wa Co-Architecture.

Picha, maelezo: Farida Khalfan


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU