Facebook Comments Box

Tuesday, June 18, 2013

RIPOTI YA MABOMU YALIYOPINGWA ARUSHA LEO

.
Arusha.

Maripota wawili wa millardayo.com kutoka Arusha wanaripoti kwamba mabomu ya machozi yakipigwa na Polisi yameanza kusikika toka saa kumi jioni kwenye eneo la Soweto.
Mmoja wa maripota hawa amesema wakati alipokua karibu na mkusanyiko huo kuna Askari Polisi mmoja ambae alijichanganya na kuingia katikati ya wafuasi wa Chadema ambao walikua wanasubiri kujua utaratibu wa kuaga miili ya Marehemu waliolipuliwa kwa mabomu na kufariki June 15 2013 na wengine zaidi ya 70 kujeruhiwa.
Baada ya hapo hawa Wafuasi hawakupenda kitendo cha Polisi kujichanganya nao hivyo ikazuka kama kutoelewana huku wakitaka atoke, baada ya dakika kadhaa huku pia Viongozi wa Chadema wakihutubia…. ndio mabomu yakaanza kusikika.
Ripota wa pili anasema “Baada ya Tundu Lissu wa Chadema kuhutubia na kusema chanzo cha vifo vya June 15 2013 ni Polisi, yani vifo hivyo viliratibiwa na RPC Arusha… mabomu ya machozi ndio yakaanza kulipuliwa”
Mpaka saa kumi na moja na dakika 40 hii post inaingia hapa, wafuasi wa Chadema bado wako maeneo ya Soweto Arusha, wamegoma kuondoka na kusema wanataka kujua kwanza usalama wa Viongozi wao…. lakini pia mabomu yanaendelea kusikika kwenye sehemu nyingine kama Sanawari, Arusha mjini, Mianzini na maeneo mengine.
 
 
 
SOURSE: MILLARD AYO


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU