Facebook Comments Box

Monday, June 3, 2013

AJALI MBAYA MOROGORO WATU WAPOTEZA MAISHA


  Foleni kubwa sana ambayoilisababishwa na ajali hiyo

 Ni Zaidi ya Kilometa 5 foleni ya Maroli na mabasi

Scania ilikuwa inaelekea Jijini Dar es salaam na Fuso ikielekea Morogoro Ziligongana uso kwa uso na kusababisha haya uyaonayo katika picha hizi.

 Zilikuwa barabarani ikalazimu zisukumwe pembeni kidogo angalau watu wapite.Ajali hiyo imehusisha FUSO lililokua linatokea Moro limesheheni mkaa,na SCANIA SEMI-TRAILER lililokuwa linatokea Dar,haya malori yamegongana,na baada ya kugongana Fuso imegeukia ilikotoka yaaan moro,na cabin ya Scania imeng'oka yote,watu watano kwenye Scania wamekufa hapohapo.

Kinachohangaikiwa sasa ni jinsi ya kuitoa hii folen ambapo magari yanayokadiriwa 3000 yamenasa kwenye foleni......
Ila inaonesha uhaba wa vifaa kama vile BREAK DOWN ndo umesababisha foleni.
Hii si ajali ya kwanza maeneo ya MASEYU,mwezi mmoja au miwili nyuma,kuna watu walibanwa na lori lililopata ajali na mmoja alikufa baada ya kushindwa kuokolewa.


 Hili Fuso inasemekana Dereva alipoteza uhai wake hapohapo na Konda ameumia sana sana.



 Kama unavyoweza kuona hapo Hata Uskani hauonekani unaweza pata picha kuwa Dereva anaweza akawa katika hali gani.


Hii ni Scania iliyogongana na Fuso hiyo waliokuwa humu wako Hospitali kwa matibabu.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU