Facebook Comments Box

Friday, May 17, 2013

MWANDISHI CHARLES MULLINDA AJITOA KWENYE JUKWAA LA WAHARIRI


8 c1dd8
Charles Mullinda


Mhariri Mtanzania Jumatano
Kaimu Mwenyekiti
Jukwaa la Wahariri
YAH: KUJITOA KWENYE JUKWAA


Napenda kukufahamisha kuwa nimeamua kujitoa kwenye Jukwaa la Wahariri kwa sababu siridhiki na mwenendo wa Jukwaa hilo.Nimeamua kujitoa kwa sababu sijaridhishwa na uamuzi uliofikiwa wa kuingilia uhuru wa habari na kufumbia macho baadhi ya mambo ambayo ninaamini hayapaswi kufumbiwa macho.
Uamuzi wangu huu pia unatokana na jinsi jukwaa linavyotumia nguvu kubwa kuficha ukweli unao wahusisha
baadhi ya wahariri ambao gazeti hili lilibaini kuwa walikuwa na mawasiliano yenye utata na aliyekuwa mtuhumiwa wa ugaidi, Joseph Ludovick. Aidha siridhishwi na jinsi baadhi ya wahariri wanavyoshambuliwa na wahariri wenzao katika magazeti yao pasipo Jukwaa kuchukua hatua huku kwa upande mwingine likitumia nguvu kubwa na pesa nyingi kuwalinda baadhi ya wahariri ambao nyendo zao zinatia mashaka.

Kikao cha kwanza na TEF na kilichofanyika leo kimedhihirisha pasipo mashaka kuwa TEF iliamua kuwa na ajenda maalumu ya kumshughulikia Mullinda kwa kuwa tu nilionyesha mawasiliano ya Deodatus Balile na Ansbert Ngurumo dhidi ya Ludovick kama ambavyo gazeti la Tanzania Daima lilivyoonyesha mawasiliano ya Dennis Msaki na Ludovick.
Ripoti ya timu iliyoundwa kuchunguza ukweli wa habari iliyoandikwa na gazeti la Mtanzania Jumatano ina upungufu mkubwa wa kimantiki ambao hata kwenye kikao niliuonyesha lakini haukusikilizwa.Ushahidi wa Ngurumo kumtumia pesa Ludovick upo wazi, lakini hakuna mtu anayeliangalia hilo kwa sababu tu timu ile iliundwa kumshughulikia Mullinda kwa sababu aliandika vigogo wa TEF ambao wako karibu na viongozi wa TEF.
Nimeamua kujitoa baada ya kubaini kuwa jukwaa linafanya kazi kwa ajili ya maslahi ya watu binafsi.
Kwa taarifa hii naamini utaratibu wa kawaida wa kuagana utazingatiwa.

Charles Mullinda.
 


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU