Facebook Comments Box

Friday, May 10, 2013

MGOMO WA DALADALA WAITIKISA IRINGA LEO

Huko mjini Iringa, daladala za Manispaa hiyo zimegoma kufanya biashara leo kutokana na  kile  wamiliki na madereva  wanachodai ni kuchoshwa na manyanyaso ya Afisa mpya wa SUMATRA wa mkoa wa Iringa.

Francis Godwin katika blog yake anasema kiini cha mgomo huo ni kinatokana na kuchukizwa na uamuzi  wa SUMATRA mkoa wa Iringa kufuta stendi ya Posta pamoja na kuzuia daladala kukaa kwa muda katika eneo la stendi ya daladala ya Miyomboni maeneo ambayo walikuwa wakikaa siku zote, hivyo, madereva  hao wamesema hawatafanya kazi hadi hapo SUMATRA Iringa itakapofuta maagizo yake hayo.
Picture
Picture
Picture



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU