Facebook Comments Box

Sunday, May 12, 2013

MAJESHI YA TANZANIA YAFIKA DRC CONGO

 
Umoja wa Mataifa (UN) umearifu kwamba kundi la kwanza la wanajeshi (TANZBATT 1-DRC) 100 kutoka nchini Tanzania limewasili Jumamosi hii katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) katika mpango wa amani wa UN wa kukabiliana na makundi ya waasi.

Tanzania inatarajia kupeleka jumla ya wanajeshi wake 1,280 katika mpango huo.

Hatua hiyo ni utekelezaji wa azimio la Machi 28 lililopitishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, UNSC wa kuunda brigedi maalumu ya kupambana na waasi katika eneo la mashariki mwa DRC.

Msemaji wa mpango huo Felix Basse amesema Tanzania imekuwa ni nchi ya kwanza kupeleka wanajeshi wake katika eneo hilo, wanajeshi zaidi toka Malawi na Afrika Kusini wanaarajiwa kujiunga na kikosi hicho wakati wowote kuanzia hivi sasa.

Wanajeshi zaidi ya 3,000 watadhibiti makundi ya waasi zaidi ya 25 katika mkoa wa Kivu pekee. Tayari kundi la waasi la M23 limeripotiwa kujiandaa ili kujibu mashambulizi yatakayoelekezwa kwao na vikosi hivyo.

Jeshi la DRC kwa muda mrefu limeshindwa kutokomeza makundi la waasi katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo, hata hivyo mamlaka za nchi hiyo zinatarajia mpango wa sasa wa UN huenda ukazaa matunda mema kwa usalama wa nchi hiyo.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU