Facebook Comments Box

Saturday, April 6, 2013

MALAWI WAAMBIWA WAACHE KUTAPATAPA


 
Waziri wa mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe (wapili kutoka kulia) akizungumza na waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam kuhusu tamko la Serikali juu ya mgogoro wa mpaka wa ziwa Nyasa. 

SERIKALI ya Tanzania imeomba  Malawi iache kutapatapa kuhusu mgogoro wa mipaka wa ziwa Nyasa kufuatia Rais  wa nchi hiyo, Joyce Banda kutangaza katika  baadhi ya vyombo vya  habari  kuwa atapeleka  suala hilo kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Haki(ICJ), badala yake isubiri uamuzi wa jopo la usuluhishi lifanye kazi na litoe maamuzi.
Aidha serikali  imesema kuwa hata siku moja  haijapelekewa taarifa wala nyaraka za siri kutoka kwa Katibu wa jopo hilo, ambalo linahusisha marais wastaafu wa zamani wa Afrika na wanasheria  kama ilivyodaiwa  na  Rais  Banda katika vyombo hivyo , kuwa kuna Mtanzania anayeitwa Dk. John Tesha ambaye wanaamini ametoa  habari na kuiba nyaraka za siri.
Akilitolea ufafanuzi   jambo hili, Waziri Membe amesema kuwa  Tanzania na jopo hilo   limestushwa juu ya madai hayo na hatua ya Rais Banda kupoteza imani.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU