Facebook Comments Box

Thursday, April 18, 2013

BI KIDUDE AZIKWA NA UMATI WA WATU ZANZIBAR


Jeneza la bibi likielekea msikitini kwa ajili ya kuswaliwa
 
Jeneza lenye Mwili wa Msanii mkongwe wa Muziki wa  Taarab, Marehem Fatma Bint Baraka Khamis(Bi Kidude) likitolewa katika msikiti wa Mwembeshauri aliposwaliwa mchana wa leo kabla ya kwenda kuzikwa.

 Taratibu za Mazishi zikiendelea kama inavyo onekana katika picha
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein akiweka udongo katika kaburi la Msanii mkongwe wa Taarab Tanzania, Fatma Baraka (Bi Kidude) katika makaburi ya Kitumba Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja. 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete akiweka udongo katika kaburi la Msanii mkongwe wa Taarab Tanzania, Fatma Baraka (Bi Kidude) Katika makaburi ya Kitumba wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif akiweka udongo

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq akiweka udongo.
Mtangazaji Hassan Bond, Fid Q, Diamond Platnumz na Ruge Mutahaba wakiwa msibani nyumbani kwa marehemu bi Kidude,  Zanzibar
Msanii Fid Q, Baraka cousin ya Marehemu Bi Kidude na Hassan Bond Mussa (FID Q ndo alikuwa msanii wa kwanza mkubwa kufika msibani kwa bibi)
Ruge mutahaba, Babu Tale and Guru. .......msibani kwa Bi Kidude

Hassan na Fid Q wakiwa katika picha ya pamoja na familia ya Marehemu Bi Kidude
Sehemu ya umati wa Watu waliofika msibani







Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU