Facebook Comments Box

Wednesday, March 13, 2013

MCHUNGAJI AKAMATWA MKOANI RUKWA KWA TUHUMA YA UCHOCHEZI WA KIDINI

Mchungaji Christopher Mtikila

Polisi mkoani Rukwa imemkamata na kumuhoji mwenyekiti wa chama cha Democtaric Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila kwa tuhuma za uchochezi wa kidini baina ya wakristo na waislam.
Mtikila ambae yupo mkoani Rukwa kwa takribani wiki mbili amekamatwa baada ya kuitisha kongamano la wachungaji na viongozi wa kidini wa kikristo mjini Sumbawanga
Katika kongamano hilo Mtikila anadaiwa alihamasisha uchochezi uliokuwa na viashiria vya uvunjifu wa amani
Kamanda wa Polisi Mkoani Rukwa Jacob Mwaruanda anadai kuwa katika kongamano hilo Mtikila aliwaambia wakristo wamekuwa wakionewa na waislam kwa muda mrefu. Na akiwahamasisha wakristo wawavaimie waislam

SOURSE: HABARI LEO

Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU