Facebook Comments Box

Friday, March 15, 2013

IKO WAPI KAMATI YA MARIDHIANO ZANZIBAR?

- Inawezekana kuwa imetekwa nyara
- Au Haitambui majukumu yake. 
Wale wanaofahamu dhana nzima ya kuanzishwa Kamati ya Maridhiano Zanzibar umefika wakati wa kujiuliza IKo wapi kamati ya Maridhiano?
Amma kwa wale wasiofahamu dhana na chimbuko la kuanzishwa kamati ya maridhiano wao watasema kamati hii ipo.
Ni vyema kufahamu chimbuko la dhana ya Kuweko Kamati ya Maridhiano. Baada ya miongo ya misuguano ya kisiasa Zanzibar juhudi kadhaa zilichukuliwa kurudisha imani miongoni mwa Wazanzibar ili kuendeleza siasa chini ya misingi ya demokrasia, haki, usawa, pamoja na kutii sheria za nchi huku tukidumisha usalama, umoja na amani.
Juhudi zilizaa matunda mwaka 2009, baada ya maridhiano yaliyofikiwa baina ya vyama vya CCM na CUF na kuamua kufuta uhasama yaliyosimamiwa na wajumbe kutoka pande zote mbili. Mwanzoni yalikuwa mazungumzo yaliyoendeshwa kwa siri kubwa hadi pale ilipofika time ya kuyatangaza, viongozi wakuu wawili waliyabariki, kuyakubali na kuyaridhia.
Kilichofuata ilikuwa ni “Road map” kuelekea dhamira thabiti ya maridhiano haya ikiwa ni pamoja na kuliomba Baraza la Wawakilishi kujadili dhana nzima, pale itakapoonekana    inawafiki maridhiano haya yasimamiwe kikatiba. Halkadhalika maamuzi yote lazima yasimamiwe na wananchi wenyewe kwa kupiga kura ya maoni kukubali au kukataa.
Hivyo basi, Kamati ile iliyoasisi maridhiano ilikabidhisha mamlaka yake kwa Baraza la Wawakilishi. Wakati wa mjadala, Baraza la Wawakilishi liliunda kamati, ambayo ndio iliyosimamia hadi kuhitimisha maridhiano na kuikaribisha Serikali  ya Umoja wa Kitaifa.
Hapo utaona hadi kukamilika kwa maridhiano kulitokana na kamati mbili; i) kamati ya kuasisi maridhiano na (ii) kamati ya kusimamia maridhiano.
Hapa ndio dhana ya kuendelea kuwa na Kamati ya Mridhiano ilipoanzia. Kuona kwamba ili Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar iweze kudumu na kutatua vikwazo vitakavyojitokeza lazima kuwe na upande mwengine (third party). Upande huu utakuwa suluhishi wa mizozo pindi ikijitokeza. Vilevile utakuwa ndi muelekeo (dira) kuielekeza serikali pamoja na kuwa kunganishi kwa wananchi.
Kwa vile haya ni maridhiano bila ya shaka kulikuwa na uhasama, hivyo suala la usuluhishi na kusameheana lilipaswa lipewe nafasi yake. Kuorodheshwa na sera za kitaifa na kutengwa zile sera za kivyama ilikuwa ndio uti mgongo wa Kamati ya Maridhiano.
Haya yote yalitakiwa kufanywa na ile kamati iliyoundwa na Baraza la Wawakilishi kwani imetokana na chombo cha kutunga sheria, imechaguliwana wananchi pia inajumuisha wajumbe kutoka vyama vyote viwili (CCM  na CUF).
Kinyume chake ile kamati ya Waasisi ndio iliyojichukulia na kujitwisha kama ndio Kamati ya Maridhiano. Hili limepelekea kukosa utendaji na kupoteza muelekeo wa dhana nzima ya kuwa na Kamati ya Maridhiano.
Kuna haja ya kufikiria kuundwa upya wa Kamati ya Maridhiano ili iweze kufikia lengo la kuweko kwake. Zanzibar inahitaji sera za kitaifa, umoja, suluhu (reconciliation),   nani mwengine kama sio uimara wa Kamati ya Maridhiano.

SOURSE: MZALENDO NET


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU