Facebook Comments Box

Saturday, February 9, 2013

WABUNGE WATAKAO KATAA KUHOJIWA NA KAMATI WATAKAMATWA NA POLISI

Bunge limesema wabunge watakaokataa kuhojiwa na Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge, watakamatwa na polisi na  kufikisha kwenye kikao cha kamati hiyo.

Juiz, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia  na Maendeleo (CHADEMA), Dk Wilbroad Slaa aliwakataza wabunge wake kuitika wito wa kuhojiwa na kamati hiyo hadi Spika atakapojibu  baadhi ya madai ya chama hicho.

Akizungumza na NIPASHE jana, Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge, John Joel, alisema  mbunge anayehitajika kuhojiwa na kamati hiyo hupelekewa barua ya kuitwa na endapo akikataa kufika atakamatwa na  polisi.
“Mbona jambo hili lipo wazi kwa kila mbunge kwa kuwa sheria zinajieleza kuwa ukikataa wito utafuatwa na askari ambaye atakuleta kwa lazima katika kamati hii.
Dk Slaa alikataa wabunge kuhojiwa baada ya  Spika wa Bunge, Anne Makinda, kuitaka  Kamati ya Maadili  kuchunguza vurugu zilizojitokeza  wiki wakati wabunge walipokuwa wakijadili hoja binafsi ya Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), iliyohusu upatikanaji wa majisafi na uondoshaji wa majitaka  Dar es Salaam.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU