Facebook Comments Box

Monday, February 11, 2013

MAPIGANO MAKUBWA GEITA KATI YA WAISLAM NA WAKRISTO


Taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema kumetokea mapigano makubwa Geita eneo la Buseresere baina ya Waislam na Wakristo chanzo cha mapigano hayo ni wakristo kuanza kuchinja nyama na kuiuza.
Chanzo chetu kinaarifu mpaka sasa msikiti umesha chomwa moto na polisi bado hawajafika kwa kuhofia uchache wao kwa hiyo wameagiza polisi kutoka Mkoa wa Mwanza waje kuwasaidia kutuliza ghasia hizo.
Silaha zinazotumika ni silaha za jadi watu wanazunguka mtaani wanakukamata wanakuuliza jina ukitaja jina tofauti na imani yao unapigwa kiasi cha kutosha tu
Kwa mujibu wa Taarifa hizo tayari idadi ya watu 10 wamejeruhiwa kwa kukatwa mapanga ambapo mmoja hali yake inaelezwa kuwa mbaya na amekimbizwa ktika hospitali ya wilaya ya geita,tayari polisi wa kikosi maalum cha kutuliza ghasia FFU kikiongozwa na Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai mkoani Geita wamewasili eneo la tukio.
Wakristo hao walifanya mkutano wa hadhara jana na kusema kuanzia leo hawatakubali kula nyama  iliyochinjwa na waislam. Na kutenga eneo lao maalumu la kuchinji nyama zao

Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU