Facebook Comments Box

Friday, January 11, 2013

POLISI WAKAMATWA WAKISAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA



Picha hii na Maktaba.

ASKARI polisi wawili wa wilayani Bunda, mkoani Mara, wanashikiliwa na jeshi la polisi katika mkoa wa Simiyu, kwa tuhuma ya kusafirisha madawa ya kulevya aina ya mirungi.

Kamanda wa polisi mkoani Simiyu Salum Msangi, amesema kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 7:30 mchana, katika kizuizi cha polisi kilichoko katika eneo la wilaya ya Busega, karibu na mji mdogo wa Lamadi, kwenye barabara kuu ya Mwanza-Musoma.

Kamanda Msangi amewataja asakari polisi hao kuwa ni pamoja na mwenye namba E. 4640 koplo Daniel na E. 6224 Koplo Mwinyihaji, na kwamba walikamatwa wakiwa na mirungi yenye uzito wa kilo 72 iliyokuwa imewekwa kwenye mabegi mawili.

Alisema kuwa askari hao walikuwa na gari binafsi yenye namba T. 168 DWB, aina ya Noah, ambapo pia walikuwa na wanawake wawili, Achien Aoko (30) na Penina Samson (20), ambao wote ni wakazi wa wilayani Tarime.

Aidha, alisema kuwa baada ya askari hao ambao walikuwa wamevaa kiraia kufika katika kizuizi hicho, gari yao ilipekuliwa na askari, na ndipo ikagundulika kwamba kulikuwa na mabegi mawili ya mirungi.

Kamanda Msangi alisema kuwa askari hao tayari wanaendelea na mashitaka ya kijeshi, ambapo wanawake waliokuwa nao jana wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Bariadi ambayo kwa sasa inafanya kazi kama mahakama ya mkoa wa Simiyu.




Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU