Facebook Comments Box

Wednesday, January 30, 2013

IGP MWEMA APATA AJALI MBAYA MOROGORO


                                               IGP SAID MWEMA


Jinamizi la ajali  limeendelea  kuwaandama viongozi  wa  juu  serikali na vyama baada ya  juzi waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa kunusurika kifo katika ajali  iliyotokea eneo la Bwawani mkoani Morogoro  ,Mkuu wa jeshi la polisi nchini (IGP )  Said Mwema leo amenusurika  kifo  baada ya gari lake alilokuwa akisafiria  kupinduka.
Ajali  hiyo  imetokea  majira ya mchana katika  eneo Mkundi Manispaa ya Morogoro wakati kiongozi huyo akitokea  jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Dodoma.
Hata  hivyo katika ajali  hiyo hakuna madhara makubwa kwa  binadamu zaidi ya gari  kuharibika  kiasi na msafara  wa  IGP kuendelea na safari  ya Dodoma kwa  kutumia usafiri mwingine .


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU