Facebook Comments Box

Tuesday, September 25, 2012

ZIMWI LA YANGA LAIKUTA COAST UNION. KOCHA WAO KIBARUA CHAOTA NYASI

Juma Mgunda akiokolewa na polisi kuondoka uwanjani kwa amani baada ya mechi ya Bandari
Baada ya kunusurika kupigwa na mashabiki katika mechi ya kirafiki dhidi Bandari ya Mombasa, na kuendelea kupewa presha kubwa na mashabiki wa timu yake ya Coastal Union hatimaye kocha wa klabu hiyo yenye maskani yake jijini Tanga Juma Mgunda ametangaza kujiuzulu kuifundisha timu hiyo baada kuiongoza timu kwenye mechi zisizozidi nne kwenye ligi kuu ya Tanzania bara.

Mgunda ambaye alipewa kibarua cha kuifundisha Coastal Union kipindic ha kiangazi kilichopita amesema ameamua kujiuzulu kutokana na presha kubwa anayopewa mashabiki kiasi cha wengine kutishia usalama wake.

Mgunda ameiongoza Coastal katika mechi 3 za ligi, akishinda moja na wakitoa suluhu mechi mbili.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU