Facebook Comments Box

Friday, January 9, 2015

BABA AJINYONGA BAADA YA KUMTOBOA MTOTO WAKE MACHO

Mtoto Agripina
Mkazi wa Muleba mkoani Kagera Godfrey Joseph Kajuna mwenye miaka 45 amejinyonga mpaka kufa baada ya kumshushia kipigo kikali na kumtoboa macho binti yake Agripina Godfrey mwenye miaka 12.

Bwana Godfrey aliondoka nyumbani kwake akiacha maagizo kuwa wasimfungulie mlango mama yao pindi akirudi nyumbani. Mabinti hao aliporudi mama yao hawakufungua mlango kwa kumuhofia baba yao.

Baba yao aliporudi aliuliza mama yao yupo wapi. Ndipo watoto hao wakamjibu kuwa ameenda kujihifadhi sehemu nyingine kwa kuwa hawaku mfungulia kama maagizo yake aliyo yaache. Baada ya maelezo hayo Bwana Godfrey alianza kumpiga binti huyo ambae ni mkubwa hapo nyumbani na kumtoboa macho.

Baada ya kutenda kitendo hicho bwana Gedfrey alijinyonga akiacha ujumbe kuwa anaogopa kukamatwa kutokana na kitendo hicho na vitendo vingine ambavyo amekuwa akiifanyia familia yake.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU