Facebook Comments Box

Monday, August 11, 2014

PUNGUZENI FURAHA WANA ARSENAL;HATA MWAKA JANA TULIANZA HIVI

Mabingwa wa ngao ya jamii
Habari wana Arsenal wenzangu, Mmeuchukuliaje ushindi wa jana dhidi ya Manchester City. Bado furaha ipo mpaka leo? Umekuwa hauna stori nzuri kuhadithia wenzako kazini zaidi ya mechi ya jana na bao zuri la Giroud?Bado ukiipamba stori yako na vijimaneno kama vile "kumbuka hawa ndio mabingwa wetu wa EPL msimu uliopita". Sitaki kusema ushindi wetu jana ulikuwa wa bahati, ule ni ushindi mjarabu katika wakati halisi.

Baadhi ya watu wasioipenda Arsenal wanasema Manchester City isingeweza kushinda kutokana na kikosi chao kutokuwa na baadhi ya wachezaji wao nyota huku wakisahau kuwa Arsenal nao hawakuwepo wachezaji nyota wengine katika mechi hiyo. Na kwa vile tumeshinda na Ngao tunayo sie hatunabudi sisi kuwa waongeaji na ikiwezekana kuwakejeli tutakavyo.

Kinachonirudisha nyuma hapa ni historia ya msimu uliopita. Kama una kumbukumbu nzuri mwaka jana wiki moja kabla ya ligi tulicheza mechi ya kirafiki na Manchester City tukawafunga tukawa na matumaini na kikosi chetu lakini kuingia kwenye ligi Manchester City wakawa mabingwa. Kwahiyo furaha yetu tusiendeleze mpaka kwenye ligi iishie pale huku tukiangalia mwenendo wetu katika ligi.

Msinichukie wala kunielewa vibaya sisemi kuwa Arsenal itafanya vibaya msimu huu maana mimi ndio niliandika kuwa msimu huu ndio kila mshabiki wa Arsenal atakuwa na furaha. Kusema itafanya vibaya itakuwa unafiki ila nnacho waambia tusihesabu kuku kwa mayai yaliyotagwa jana tuwe na subira na tusubiri yaanguliwe mayai.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU