Facebook Comments Box

Wednesday, June 18, 2014

TANZANIA YAPIGA MARUFUKU UVUTAJI WA SHISHA

Uvutaji wa Shisha ni sawa na uvutaji wa sigara kulingana na
madaktari
Serikali ya Tanzania imepiga marufuku uvutaji wa Shisha.
Uraibu huo unaohusisha uvutaji wa Tumbaku yenye ladha tofauti
tofauti ambayo hutiwa ndani ya chupa kubwa na kuvutwa kwa
mirija, umeshika kasi sana Tanzania hasa miongoni mwa vijana
wadogo mjini Dar Es Salaam.
Baadhi ya watu wanaiona Shisha kama isiyokuwa na madhara ya
kiafya ikilinganishwa na uvutaji wa Sigara.
Lakini wataalamu wanaamini kuwa uvutaji wa Shisha kwa muda wa
saa moja ni sawa na kuvuta sigara miamoja.
Madaktari walitoa onyo kuhusu uvutaji wa Shisha wanakabiliwa na
tisho la kuugua Saratani sawa na hatari inayowakabili wavutaji wa
sigara.

 CHANZO: BBC


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU