Facebook Comments Box

Monday, December 2, 2013

AZAM TV KUANZA KURUSHA MATANGAZO DESEMBA 6: ANGALIA PICHA ZA UZINDUZI ULIVYO KUWA

IMG_6374
Mtangazaji wa Televisheni ya Azam TV Wasiwasi Mwabulambo akiwa kwenye Red Carpet kabla ya mahojiano na Mkurugeni wa Kajunason Blog Cathbert Angelo.
IMG_6378
Afisa Mtendaji Mkuu na Mbunge wa Singida Mjini Mh. Mohammed Dewji alikuwa ni miongoni mwa wageni waalikwa kwenye uzinduzi wa Azam TV. Pichani akifanya mahojiano na Mtangazaji wa Azam TV Wasiwasi Mwambulambo.
IMG_6379
IMG_6405
Mtangazaji wa Azam TV Wasiwasi Mwabulambo akifanya mahojiano na Mdau William Malecela a.k.a LEMUTUZ na Mmiliki wa Blog ya Wananchi.
IMG_6505
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. January Makamba (MB) akizungumza kwenye uzinduzi wa Azam TV uliofanyika Hyatt Regency The Kilimanjaro Hotel mwishoni mwa Juma ambapo amesema Azam TV imekujali kuleta mapinduzi katika ulimwengu wa Digitali na kutoa fursa ya ajira kwa Vijana wa Tanzania wenye vipaji sanjari na kuitangaza nchi yetu katika bara la Afrika hasa kwenye upande wa Soka na Filamu.
Azam TV itaanza kurusha matangazo yake Desemba 6 mwaka huu, Watanzania kaeni mkao wa kula kupata King’amuzi kwa bei rahisi ambacho kitakuwa na chaneli zisizopungua 50.
IMG_6513
Fashi fashi zikipamba uzinduzi rasmi wa Azam TV.
IMG_6518
Baadhi ya wafanyakazi wa Azam TV kitengo cha Huduma kwa Wateja wakiwa wameshikilia Ving’amuzi vya Azam TV wakati wa uzinduzi huo.
IMG_6537
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. January Makamba (MB) akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa Azam TV mara baada ya kuzindua rasmi kwenye sherehe zilizofanyika mwishoni mwa Juma Hyatt Regency The Kilimanjaro Hotel.
IMG_6426
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. January Makamba (MB) katika tete-a-tete na Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media Ltd. Rhys Torrington mara baada ya kuzindua Azam TV itakayoanza kurusha matangazo yake hewani Desemba 6 mwaka huu.
IMG_6456
Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Tv, Rhys Torrington akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi rasmi wa Azam Television jijini Dar es Salaam mwishoni mwa Juma.
IMG_6478
Mkurugenzi wa vipindi wa Azam Tv Efe Atiyio akifafanua juu ya program mbalimbali za Azam Tv .Na MO BLOG
IMG_6431
Yusuf Bakhresa akizungumza jambo na watoto wake kwenye uzinduzi huo.
IMG_6415
Mkurugenzi wa kampuni ya Jambo Concepts Limited, Benny Kisaka (katikati) alikuwa miongoni mwa wageni waalikwa.

IMG_6429
Wageni waalikwa wakibadilishana mawazo wakati wa uzinduzi huo.
IMG_6422
Yusuf Bakhresa akibadilishana mawazo na wadau wa michezo nchini waliohudhuria uzinduzi huo.
IMG_6494
Mkurugenzi Mtendaji wa Aggrey & Clifford Bw. Rashid Tenga naye alikuwa ni miongoni mwa wageni waalikwa.
IMG_6460
Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Bw. Boniface Wambura (kushoto) akifuatilia yanayojiri kwenye uzinduzi huo.
IMG_6419
IMG_6484
IMG_6391
Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mh Mohammed Dewji (MB) akifurahi jambo na wadau.
IMG_6388
IMG_6414
IMG_6571
Mtangazaji maarufu wa Radio One na ITV Maulid Kitenge na Mfanyabiashara maarufu CEO wa Delina Group Enterprises Bw. Davis Mosha wakifurahi jambo wakati wa uzinduzi huo.
IMG_6492
Pichani juu na chini ni baadhi ya wadau waliohudhuria uzinduzi huo.
IMG_6497
IMG_6398
IMG_6421
IMG_6463
IMG_6427
IMG_6589
Mkurugenzi Mkuu wa makampuni ya SSB Ltd. Said Muhammad Said (wa pili kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni za Bakhresa.
IMG_6586
Mdau Omar Said ( wa pili kulia) akiwa na baadhi ya wafanyakazi wenzake kwenye picha ya pamoja.

CHANZO: TANZANIA NEWS


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU