Facebook Comments Box

Saturday, August 10, 2013

TETESI: SHEIKH PONDA APIGWA RISASI MOROGORO LEO

Sheikh Ponda Issa Ponda
Habari zilizotufikia zinasema kuwa Sheikh Ponda Issa Ponda kapigwa risasi mkoani morogoro leo. Inasemkana sheikh Ponda alipigwa risasi baada ya kushuka kwenye tax kwa ajili ya kuhutubia mhadhara katika eneo la kiwanja cha ndege. Chanzo cha habari kinasema risasi hizo zimempiga bega la kushoto naa sheikh ni mzima ila chanzo kingine cha habari kinasema amepigwa risasi nyingi na huenda mauti yamemkuta. (Inna lillah wa inna illayhi rajiuun)

 RPC, Faustine Shilogile, anasema hali ni shwari ila Ponda hajui hali yake Maana polisi walizuia gari la Ponda wamkamate, lakini wananchi wakaanza kushambulia polisi ndipo wakarusha risasi hewani kutawanya watu, lakini wananchi wakamtorosha. Anasema taarifa ni nyingi za uongo, hakuna watu polisi wala hospitali waliozingira na anaomba anayejua alipo atoe taarifa.

Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU