Facebook Comments Box

Wednesday, August 14, 2013

VIDEO YA DAKTARI AKIMPIGA NGUMI MGONJWA

Daktari mmoja nchini Urusi, Andrey Votyakov (bingwa katika fani ya usingizi) mapema mwezi uliopita alitimuliwa kazi baada ya video ya chumba cha upasuaji inayorekodi matukio (surveillance camera) kuoneshwa hadharani ambapo daktari huyo alionekana akilumbana na mgonjwa aliyefungwa kitandani na baadaye kumshushia makonde usoni na kifuani, upande wa kushoto.

Mgonjwa huyo aliyekuwa katika kitendo cha magonjwa ya moyo, alikuwa wa umri wa makamo (miaka 45) na alifariki muda mfupi baadaye.

Tukio hilo lilitoea mwezi Februari mwaka huu lakini liligundulika mwezi Julai.

Daktari huyo ambaye hakuwa na rekodi yoyote mbaya kazini, alijitetea kuwa alipandwa na jazba baada ya mgonjwa kumsemea maneno yaliyomuudhi na kujikuta amempiga. Vile vile alisema uchovu uliotokana na kufanya kazi mfululizo kwa saa 24, ulichangia kushindwa kwake kufanya maamuzi yenye busara.


CHANZO: WAVUTI



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU