Facebook Comments Box

Tuesday, February 12, 2013

TFF WAOMBA YANGA WAWASHANGILIE SIMBA NA AZAM KWENYE MECHI ZA KIMATAIFA



Release No. 026
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 12, 2013

WASHABIKI WAZIUNGE MKONO AZAM, SIMBA

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawaka washabiki wa mpira wamiguu kujitokeza kwa wingi wikiendi hii kuzishangilia timu za Azam na Simbazitakazocheza mechi za mashindano ya Afrika jijini Dar es Salaam.Nguvu ya washabiki ni muhimu katika kuziweza timu hizo kufanya vizuri katikamechi hizo za nyumbani dhidi ya Al Nasir Juba ya Sudan Kusini na Club Liboloya Angola.Azam itacheza Jumamosi (Februari 16 mwaka huu) dhidi ya Al Nasir katikamechi ya Kombe la Shirikisho wakati Simba itaikabili Club Libolo kwenyemechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakayofanyika Jumapili. Mechi zotezitachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

LYON, YANGA KUUMANA UWANJA WA TAIFA
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inamalizaraundi ya 16 kesho (Februari 13 mwaka huu) kwa mechi kati ya wenyejiAfrican Lyon dhidi ya Yanga itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Mechi hiyo itakayochezshwa na mwamuzi Martin Saanya kutoka Morogoroinakutanisha timu zenye mazingira tofauti. Wakati Yanga wakiwa ndiyo vinarawa ligi hiyo kwa pointi 33, African Lyon ambayo sasa inanolewa na SalumBausi inakamata mkia ikiwa na pointi tisa tu.Nayo Toto Africans itaikaribisha Polisi ya Morogoro kwenye Uwanja wa CCMKirumba jijini Mwanza katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi JacobAdongo kutoka Musoma. Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wenye uwezo wakuchukua watazamaji 20,000 utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya MgamboShooting na Oljoro JKT.Nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Maxime ambaye sasa ni kocha waMtibwa Sugar ataiongoza timu yake hiyo katika mechi dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani, Morogoro. Ni kwenye uwanja huo ambapo Mtibwa Sugar katika mechi yao iliyopita walichapwa mabao 4-1na Azam.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU