Facebook Comments Box

Wednesday, January 9, 2013

HII NDIO SIRI YA FAST JET KUWA NA BEI RAHISI


Bei ya nauli ya chini ya fastjet yafafanuliwa
Tunajivunia kuwa shirika la kwanza la ndege linalotoa huduma kwa gharama nafuu kabisa.
Mfumo huu wa gharama nafuu katika mashirika ya ndege umekuwa maarufu sana ndani ya mabara ya Ulaya, Asia na Marekani kwa zaidi ya miaka 10. Kwa uhakika, Easyjet, ni moja kati ya mashirika ya gharama nafuu na ni shirika kubwa sana katika bara la Ulaya (ambaye mwanzilishi wake na mwanahisa mkubwa wa fastjet) na kubeba zaidi ya abiria milioni 55 ndani ya mwaka huu

Ni jinsi gani tunaweza kupata nauli chini mno?

Kuna njia kuu tatu tunazotumia kuwezesha nauli za ndege kuwa chini. Kwanza, tunaajiri watu wajanja na werevu, tunatumia mifumo na mikakati ambayo hupunguza gharama na kuongeza ufanisi wa kazi – hii hufanyika nyuma ya pazia na hutoweza kuona ikifanyika. Pia tunanunua sarafu yetu na mafuta ya ndege kabla, ili kuweka gharama zetu chini. Pia tunazingatia kwenye aina moja ya ndege, ambayo ni Airbus 319 katika kampuni yetu, hii inapunguza gharama pia kwani tuna aina moja ya vipuri na wataalamu wa ndege.
Njia mbili zingine utakazo zigundua, Kwanza, tunatumia mbinu ya 'lipia unachotumia' katika usafiri wetu wa anga.

Hii inamaanisha abiria analipia anachotumia wakati wa safari na si zaidi.

Unapolipia tiketi zetu unakuwa umelipia pamoja na siti kwenye ndege na mizigo moja wa kubeba mkononi. Kila kitu kingine cha ziada kwanzia gharama ya mizigo hadi vinywaji -  vitalipiwa kwa kutumia Mfumo wa” kulipa-kwa-matumizi”. Kama unataka chakula unaweza kulipa, na kama huhitaji chakula huna haja ya kukilipia. Katika mashirika mengine ya ndege unalazimika kulipia huduma ambazo hata hutotumia, mfano unakuta ndege zingine zina madaraja na huduma za gharama, lakini kwa fastjet tunatoa bidhaa zetu kwa gharama rahisi sana unaweza kulipia huduma Fulani kama unaitaka, kama huduma ya basi.
Njia ya tatu na mwisho tunayotumia kuifanya nauli yetu iwe chini ni kwa kuweka madaraja katika nauli zetu. Nauli zetu zinapatikana kati ya dola $ 20-150: Fanya mipango yako ya safari mapema, upate nauli ya chini. Hii inatusaidia kujaza ndege zetu (ni zaidi ya gharama nafuu) pia tunawapa fursa wateja wetu kupata bei nafuu sana, kinachotakiwa ni kufanya maandalizi ya safari mapema. Tumekuwa sana katika soko la Tanzania na tumefanikiwa kuwapa fursa maelfu ya watu ambao hakuwahi kusafiri kwa anga.
Mfumo wa Gharama nafuu ni muhimu sana kwa fastjet. Nauli zetu si tu za utangulizi, tunaahadi kuwa na nauli nafuu kadri tuwezavyo na kwa muda mrefu. Lengo letu ni kuanzisha aina ya usafiri wa anga wa gharama nafuu katika bara la Afrika kama ambavyo mabara ya Ulaya na Marekani wamekuwa wakifurahia huduma hii kwa miaka mingi.
Kusafiri kwa anga si tu kwa ajili ya matajiri na watu maarufu, Mfumo wetu wa nauli ya chini ina mpa kila mmoja fursa ya kusafiri kwa anga.

Tunapenda kuuita "Usafiri Makini"



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU