Facebook Comments Box

Monday, June 3, 2013

MAKAMU WA RAIS DKT. GHARIB BILAL AZINDUA RASIMU YA KATIBA MPYA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA LEO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiinua juu na kunyesha Kitabu cha Rasimu ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, (kushoto) ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, Joseph Sinde Warioba.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Rasimu ya Katiba mpya, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, baada ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Rasimu ya Katiba mpya, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, baada ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.  Katikati ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, Joseph Sinde Warioba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Rasimu ya Katiba mpya,Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,Balozi Seif Ali Iddi baada ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. 

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Rasimu ya Katiba mpya, Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Asha-rose Migiro, baada ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Kushoto kwa Makamu, ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Idd (kushoto) ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, Joseph Sinde Warioba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Rasimu ya Katiba mpya, Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, baada ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.  Katikati ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, Joseph Sinde Warioba.
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, Joseph Sinde Warioba akisoma hotuba yake wakati wa uzinduzi rasmi wa rasimu ya Katiba uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal kabla ya  uzinduzi rasmi wa rasimu ya Katiba uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

 Viongozi mbali mbali wakifuatilia hotuba hiyo 
 Wanahabari


 Picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal akiteta jambo na Mjumbe wa Kamati ya Katiba,Dkt. Salim Ahmed Salim.


TAIFA STARS SUDAN NGUVU SAWA


                         Kikosi cha Timu ya Taifa 'Taifa Stars'

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imetoka sare ya bila kufungana na Sudan (Nile Crodcodile) katika mechi ya kujipima nguvu iliyochezwa jana (Juni 2) kwenye Uwanja wa Addis Ababa nchini Ethiopia.

Mechi hiyo iliyochezeshwa na mwamuzi Bamlak Tessema wa Ethiopia ilikuwa sehemu ya maandalizi kwa timu zote ambazo wikiendi ijayo zinacheza mechi za mchujo za Kombe la Dunia. Wakati Stars itakuwa ugenini nchini Morocco, Sudan itacheza nyumbani dhidi ya Ghana.

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ilicheza vizuri mechi hiyo, hasa kipindi cha pili ambapo ilifanikiwa kutengeneza nafasi kadhaa za kufunga lakini ama washambuliaji walipiga nje au mipira yao kuokolewa na kipa Ehab Abdelfatahh wa Sudan.

Washambualiji wa Stars akina Khamis Mcha, Mrisho Ngasa na Amri Kiemba wakiongozwa na John Bocco walilitia msukosuko mara kwa mara lango la Sudan ambalo lilikuwa chini ya beki wa kati Nadir Eltayeb ambaye alifanya kazi ya ziada dakika ya 72 kuokoa mpira uliokuwa ukielekea wavuni.

Stars katika mechi hiyo iliwakilishwa na Juma Kaseja, Nadir Haroub/Vicent Barnabas, Shomari Kapombe, Kelvin Yondani, Aggrey Morris, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Salum Abubakar, John Bocco/Haruni Chanongo, Amri Kiemba/Khamis Mcha na Simon Msuva/Athuman Idd.

Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Joram Biswaro amewataka wachezaji wa Taifa Stars kuhakikisha wanaipeleka timu hiyo kwenye fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil.

Timu inaondoka kesho alfajiri kwenda Morocco kwa kupitia Cairo, Misri ambapo inatarajia kuwasili Casablanca saa 8 mchana.


MIMBA YA DIAMOND YAANZA KUMPELEKESHA PENNY

 
Penny akiwa hospitali.
Habari zisizokuwa na chenga kutoka kwa chanzo chetu ambacho ni mtu wa karibu wa mrembo huyo, zilieleza kwamba kufuatia hali hiyo, Penny alikimbizwa kwenye Hospitali ya Regency, Dar wikiendi iliyopita kisha  akalazwa, akachomwa sindano na kutundikiwa dripu.
 
Diamond na Penny katika pozi.
Akizungumzia hali hiyo, Penny aliliambia Bongoclantz.com  kuwa ni kweli alizidiwa usiku na alikimbizwa hospitali ambapo pamoja na mengine lakini kubwa vipimo vilionesha kuwa alikuwa na malaria.
Hata hivyo, habari tulizozipata wakati tunakwenda mitamboni zilieleza kuwa Penny aliruhusiwa kutoka hospitalini na anaendelea vizuri.

AJALI MBAYA MOROGORO WATU WAPOTEZA MAISHA


  Foleni kubwa sana ambayoilisababishwa na ajali hiyo

 Ni Zaidi ya Kilometa 5 foleni ya Maroli na mabasi

Scania ilikuwa inaelekea Jijini Dar es salaam na Fuso ikielekea Morogoro Ziligongana uso kwa uso na kusababisha haya uyaonayo katika picha hizi.

 Zilikuwa barabarani ikalazimu zisukumwe pembeni kidogo angalau watu wapite.Ajali hiyo imehusisha FUSO lililokua linatokea Moro limesheheni mkaa,na SCANIA SEMI-TRAILER lililokuwa linatokea Dar,haya malori yamegongana,na baada ya kugongana Fuso imegeukia ilikotoka yaaan moro,na cabin ya Scania imeng'oka yote,watu watano kwenye Scania wamekufa hapohapo.

Kinachohangaikiwa sasa ni jinsi ya kuitoa hii folen ambapo magari yanayokadiriwa 3000 yamenasa kwenye foleni......
Ila inaonesha uhaba wa vifaa kama vile BREAK DOWN ndo umesababisha foleni.
Hii si ajali ya kwanza maeneo ya MASEYU,mwezi mmoja au miwili nyuma,kuna watu walibanwa na lori lililopata ajali na mmoja alikufa baada ya kushindwa kuokolewa.


 Hili Fuso inasemekana Dereva alipoteza uhai wake hapohapo na Konda ameumia sana sana.



 Kama unavyoweza kuona hapo Hata Uskani hauonekani unaweza pata picha kuwa Dereva anaweza akawa katika hali gani.


Hii ni Scania iliyogongana na Fuso hiyo waliokuwa humu wako Hospitali kwa matibabu.


MMOJA WA WAANZILISHI WA JAMII FORUM (MAXENCE MELO) AWASHUKURU WATANZANIA


 Wana JF,
 Kwanza namshukuru Mungu kwa kutupa fursa ya kuishi tena (2nd chance) mimi na mdogo wangu. Mungu yu mwema kwetu.
Katika ajali hii, huwezi kutarajia kuwa tumetoka tukiwa hai na tunaendelea vema kama tulivyo sasa.

Aidha, nawashukuru wote waliotoa pole zao kwetu via JF na kututakia kupona haraka. Tunashukuru sana na tunazidi kufarijika kwa ushirikiano wenu katika maombi (na baadhi walituma michango itusaidie katika matibabu). Moderators, shukrani kwa kuendelea kulisimamia jukwaa hili kwa weledi mkubwa.

 Napenda kuwashukuru wanasiasa watatu; ndugu Zitto Kabwe, Dr. Faustine Ndugulile na Ndugu Hussein Bashe - ambao wameonyesha kujali tangu tunapata ajali hadi sasa (wanatujulia hali tunavyoendelea); hii inatia moyo na kuonyesha kujali kwao kwetu. Mungu awazidishie muendelee kuwa na moyo huu. Shukrani zetu ziende kwa wana JF wa Nzega, Mwanza na Dar; ambao wamekuwa nasi bega kwa bega tangu siku ya ajali. Ni wengi lakini inakuwa vigumu kuwataja kwenye shukrani zetu hizi bali tunapenda wafahamu kuwa tunawashukuru sana.
Tunawashukuru sana wengine wote ambao kwa njia tofauti wamekuwa wakitaka kujua tunaendeleaje kiafya na kuwajuza hapa; kutokana na mazingira tulikuwa tunashindwa kuwajibu wote lakini wengi tumewajibu kuwafahamisha kilichotokea na tunavyoendelea.
Ndugu zangu, tupo hai kwa mapenzi ya Mungu tu!

Nini kilitokea?

Inakuwa vigumu kuelezea kwa kirefu kilichotokea. Kuwa ni mwendo kasi? Sijui. Kuwa ni mkono wa mtu? Pia sijui. Kuwa ni bahati mbaya? Naweza kusema hivyo! Hatumlaumu yeyote katika hili na hatumnyooshei kidole yeyote. Kwa dereva yeyote anafahamu nini kinaweza kutokea pale 'Sterling Rod' inapokatika ukiwa katika mwendo zaidi ya spidi 80.
Yapo mengi yanaweza kuhisiwa, yapo mengi yanaweza kusemwa lakini ambacho tunaweza kukiri ni kuwa Mungu yu mwema kwetu.

Hali yetu:

Baada ya ajali, mdogo wangu ambaye pia ni member wa JF kama Chachu Ombara, alibainika kuvunjika mfupa wa kati ya kiwiko na bega mkono wa kushoto na sasa amefanyiwa upasuaji na madaktari bingwa Muhimbili, anaendelea vema.
Binafsi nilibainika kuwa na uvimbe kidogo kwenye ubongo upande wa kulia; naendelea vema namshukuru Mungu.

Mwisho: 

Ushauri wangu kwa wanaoendesha magari, wasafiri kwenye ruti ndefu na hata katika hali ya kawaida: - Kabla ya safari yoyote mwite Mungu na ujikabidhi kwake, atakuitikia kwa namna ya kipekee - Unapoendesha, funga mkanda. Hata kama umekaa siti ya nyuma (katika gari binafsi). - Ukiwa barabarani (dereva), jitahidi kuzingatia alama za barabarani; wajali madereva wengine kama ambavyo ungependa wakujali.

Nasikitika kuwa huenda nisijibu maswali ambayo labda yanaweza kujitokeza kutokana na kuwa nina matatizo ya kuumwa kichwa (kilijigonga sana chini wakati gari linapinduka) lakini naamini nikikaa vema nitarejea na aidha kujibu au nikiwa nimechelewa nitatuma PM kwa mhusika.

Asanteni sana.

Maxence
 ===================
Tokana na maoni ya wengi wa wadau wa Jukwaa La Siasa kutokua na taarifa hii mbaya ya Ajali ilipokua imetangazwa hapa, mtuwie radhi Moderators kwa maamuzi ya kuhamishia habari hii Jukwaa La Siasa toka habari na hoja Mchanganyiko.

Sunday, June 2, 2013

HUKU MWILI WA NGWEA UKITARAJIWA KUWASILI JUMANNE, MIRAJI KIKWETE ATOA FULANA ZA MSIBA

Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Bi Radhia Msuya, akiweka saini kwenye kitabu cha Maombolezo nyumbani kwa Baba Mdogo wa Marehemu Mangwea, Mbezi Beach Jijini Dar es Salaam leo.

MAMA YAKE 'NGWEA' ADONDOKA GHAFLA NA KULAZWA HOSPITALI


            Bi Denisia Mangwea.mama mzazi wa msanii Albart Mangwea
 
 Mama mzazi wa  marehemu Albart Keneth Mangwea 'NGWEA' Bi Denisia Mangwea[63] leo asubuhi ameanguka ghafla baada ya kupokea taarifa kwamba mwili wa mtoto wake Albeth umeshindwa kuwasili nchini ukitokea Afrika ya kusini.Mtandao huu leo mchana ulipokea taarifa z a tukio hilo  ambapo dada mkubwa wa Albeth Bi Magreth Mangwea alipoulizwa alithibitisha mama yake kuanguka ghafla baada ya kusikia mwili wa mpendwa mtoto wake umeshindwa kuwasili  nchini.
 
" Ni kweli leo asubuhi mama alipoamka na kusikia taarifa kuwa mwili wa mwanae hautofika tena leo Jijini Dar es Salaam kutokana na Taarifa ya Daktari kuchelewa kutolewa  alianguka kwa presha na kulazwa katika hospitali ya mkoa wa Morogoro akiendelea na matibabu, na alizinduka baadae  na anaendelea vizuri na kwamba muda wowote anaweza kuruhusiwa kutoka hospitalini hapo.



SHEIKH PONDA ISSA PONDA AUNGURUMA HUKU AKIWASIHI WAISLAMU KUWA NA UMOJA


Waumini wa dini ya Kiislam wakiwa kwenye Kongamano lililofanyika leo jijini Dar es Saalaam kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo mada mbalimbali ziliwasilishwa na masheikh. Msimamo wa waisilamu juu ya Maendeleo ya mchakato wa katiba mpya, Dhulma na uonevu dhidi ya waislam pamoja na hatua za kuchukuwa kama madai yao yatapuuzwa.      

Imamu wa Msikiti wa Mtambani Imam Suleiman akimkaribisha Sheikh Ponda kuhutubia waislam kwenye Kongamano hilo.
Takbirrr zikafuatia baada ya kukaribishwa Sheikh Ponda.
Sheikh Konda Juma Bungo nae aliwasilisha mada.
Sheikh Ponda Issa Ponda  (kushoto) akihutubia waislam kwenye kongamano hilo.
Sheikh Ally Basaleh nae hakusita kuwasilisha mada kama anavyoonekana pichani.
Amiri wa Jumuia na Taasisi za Kiislam Tanzania Sheikh Musa Kundecha nae aliwaambia waislam kuwa kwa kawaida mtu akilala ukimwamsha huamka lakini ukimwona amelala una mwamsha na haamki basi ujue hajalala ila anajifanya amelala dawayake ni kumkera mpaka aamke.
Jopo la Masheikh wa Meza kuu
Waumini wa dini ya Kiislam leo wametoa msimamo juu ya masuala mbalimbali yanayoendelea nchini wakati wa kongamano lililoandaliwa na jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania jijini Dar es Salaam.
Kwenye kongamano hilo ambalo masheikh mbalimbali wakiwemo Sheikh Ponda Issa Ponda, Ally Basaleh, Mussa Kundecha na Kondo Juma Bungo waliwasilisha mada mbalimbali pamoja na kutangaza maazimio ya kongamano hilo.
Moja ya mambo yaliyozungumzwa ni mapendekezo waliyowasilisha kwenye Tume ya katiba mpya ambapo walisema iwapo mapendekezo waliyowasilishwa hayakuzingatiwa na kutupwa yote basi waisilamu watatangaza kusimamisha mchakato huo nchi nzima na kufanya maandamano usiku na mchana.
Hoja hiyo ilikuja baada ya kunukuliwa kauli ya Waziri wa nchi Sera na Uratibu wa bunge Wiliam Lukuvi, wakati akijibu swali la Mbunge Asumta Mshama aliyetaka kujua kwamba lini serikali itaacha kupanga siku ya kupiga kura kuwa Jumapili wakati wanajua siku hiyo ni siku ya ibada ya wakristo haioni inawadhulumu hakiyao yakufanya ibada?, Lukuvi kwenye jibu lake alisema suala hilo limekuwa likilalamikiwa na watu wengi tu lakini serikali kwenye hilo haina utaratibu maalum wa siku ya kupiga kura ila kwakuwa kuna mchakato wa katiba mpya hilo litazingatiwa.
“Hii ni kinyume kabisa na utaratibu wa tume ya katiba waziri huyu anataka tuamini kwamba  anayafahamu yatakayokuwemo kwenye katiba mpya kabla hata wananchi hawajapelekewa na hata haijaandikwa? Hivyo iweje waislam wanaodai siku ya ijumaa iwe ya mapumziko kwa miaka nenda rudi hawapewi wakristo wanakosa sikumoja tu ndani ya miaka mitano majibu yanapatikana kirahisi?” Alihoji sheikh Ponda.
“Waislam wamekuwa wakiomba ruhusa kwa mabosi wao siku ya ijumaa kwenda kufanya ibada na mara nyingine wananyimwa ruhusa hiyo lakini hakuna vurugu yeyote waliofanya na wanadai haki hiyo kwa miaka yote hii lakini hawapewi lakini wengine wanadai kirahisi na kujibiwa kwa uhakika.” Alifafanua.
Aidha heikh Ponda alifafanua kuwa waislam wavumilie wasubiri rasimu itakapotangazwa kwenye magazeti ya serikali kama mapendekezo waliyowasilishwa yatapuuzwa basi hakuna katiba mpya maandamano usiku na mchana mpaka kieleweke nchi nzima.


Saturday, June 1, 2013

MANJI: NGUVU YA YANGA SASA IMEELEKEZWA KWENYE UJENZI



Uongozi wa Yanga umesema umeelekeza nguvu zake katika kuanza ujenzi wa Uwanja wao wa kisasa kwenye eneo la Kaunda jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji amesema wamekuwa wakiendelea na mchakato huo na mambo yatakapokamilika, kazi ya ujenzi itaanza.
“Usione tuko kimya, mchakato unaendelea nasi tunahitaji muda kwa ajili ya kujadili, kujipanga na baadaye kuanza.

“Kamati inayohusika na masuala hayo inaendelea tunakutana na wahusika na kujadili halafu tunaangalia nini kinaendelea na nini tuendelee nacho.


“Hivyo mnatakiwa kuvuta subira na baadaye mtaona mambo yanaendelea,” alisema Manji.

Tayari uongozi Yanga ulishateua kamati inayoshughulikia suala hilo iliyo chini ya Ridhwani Kikwete.

Lakini kampuni inayohusika na ujenzi wa uwanja huo kutoka China, ilishakabidhi ramani tatu kwa Yanga na wanatakiwa kuchagua moja ambayo itumike na ujenzi.


SOURSE: SALEH JEMBE


KAMA UNAMKUMBUKA KIBAKULI SASA HIVI YUPO HIVI

DSC00429Unamkubuka jamaa anaitwa Sadiki Mberwa maarufu kama Kibakuli, alikuwa staa kwenye maigizo ya Kaole kama mtoto mnoko wa Muhogo mchungu ambaye anajua kama baba yake ana nyumba nje lakini hamwambii mama yake mzazi. Mwisho wa siku na yeye anakuja kumtaka kimapenzi mama yake mdogo.

Kikubwa kilichokuwa kinamtamburisha Kibakuli ulikuwa ubonge wake, tofauti na sasa amekuwa mwembamba na amekuwa mtu mzima. Kibakuli alianza kuigiza kwenye miaka ya 1999 yupo darasa la sita wakati akiwa na Nyamayao ambaye alikuwa anaigiza kama dada yake. Hivi sasa Kibakuli ni soundman wa Landline Production na soon atarudi tena mbele ya camera. 
k
Kibakuli


YANGA NA SIMBA HATIHATI KUSHIRIKI KAGAME

Siku kadhaa baada ya Baraza la Vyama vya soka Afrika Mashariki na Kati - CECAFA kuidhinisha michuano ya kombe la Kagame kuchezwa mjini Darfur -Sudan, serikali ya Tanzania imetoa tamko kuhusu timu za Simba na Yanga kwenda kushiriki michuano hiyo huko Sudan kwenye eneo ambalo limekuwa likiandamwa na vurugu kwa miaka kadhaa sasa.
 Kwa mujibu wa msemaji wa klabu ya Simba Ezekiel Kamwaga ni kwamba serikali haidhani ni busara kwa vilabu vya Simba na Yanga kwenda kwenye eneo hilo kushiriki Kagame Cup kutokana hali mbaya ya usalama iliyopo Darfur.
HIVI NDIVYO ALIVYOANDIKA KAMWAGA KWENYE UKURASA WAKE WA FACEBOOK.
 


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU