Monday, August 29, 2016
VITUO VIWILI VYA REDIO VYAFUNGIWA KWA MUDA USIO JULIKANA LEO
Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye amezifungia radio mbili kwa muda usiojulikana kwa makosa ya kuandaa vipindi ambavyo vimerushwa hewani vikiashiria uchochezi.
Nape amesema kuwa uamuzi wa kuvifungia vituo hivyo umefikiwa baada ya kujirdhisha kuwa kipindi cha Matukio kilichorushwa Agosti 25, 2016 muda wa saa 2 usiku hadi saa 3 na Radio 5 pamoja na kipindi cha Morning Magic katika kipengele cha Kupaka Rangi Agosti 17 vilikuwa na maudhui ya uchochezi ambao ungeweza kuleta uvunjifu wa Amani.
Amesema kuwa kufuatia tukio hilo amevifungia viyuo hivyo kwa muda usiojulikana kwani wamekiuka masharti ya kanuni ya 5 (a,b,c na d), kanuni ya 6(2a, b na c) na kanuni ya 218 ya huduma za utangazaji ya mwaka 2005.
PROF. LIPUMBA NA MAGDALENA SAKAYA WAVULIWA UANACHAMA CUF
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha CUF, Prof. Haruna Lipumba  
Chama Cha
 Wananchi (CUF) kimewasimamisha uanachama aliyekuwa Mwenyekiti wa chama 
hicho, Profesa Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu wa chama hicho upande wa 
Bara, Magdalena Sakaya.
Uamuzi 
huo umetolewa jana na Baraza Kuu la Chama hicho lililofanya mkutano wake
 visiwani Zanzibar kwa lengo la kuwajadili wanachama kadhaa wakiwemo 
vigogo hao. Sakaya amevuliwa nyadhifa zote ndani ya chama kabla ya 
kusimamishwa.
Taarifa 
kutoka ndani ya Mkutano huo zimeeleza kuwa Baraza hilo limewaadhibu 
wanachama 15 wakiwemo Sakaya ambaye pia ni mbunge wa Kaliua.
Mbali na 
vigogo hao, wengine waliopigwa rungu na Baraza Kuu la CUF ni pamoja na 
Katibu wa Baraza la Wazee, Shashi Lugeye, Thomas Malima na Naibu 
Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano, Abdul Kambaya.
Aidha, 
Baraza hilo limemsimamisha uanachama Mbunge wa Mtwara Mjini, Maftah 
Nachuma. Hatua hii inaweka matatani ubunge wa Sakaya na Nachuma kwani 
wakifikia hatua ya kufukuzwa watakosa sifa za kuendelea kuwa wabunge.
Lipumba 
na Sakaya hawakupata nafasi ya kujitetea kutokana na kutohudhuria 
mkutano huo wakati Shashi alipata nafasi ya kujitetea kutokana na uwepo 
wake lakini utetezi wake haukuzaa matunda. Katiba ya chama hicho haiwapi
 nafasi wabunge hao kukata rufaa kutokana na uamuzi wa Baraza hilo.
Uamuzi 
huo umekuja ikiwa ni siku chacha baada ya Mkutano Mkuu Maalum wa Chama 
hicho uliolenga kumchagua Mwenyekiti Mpya kuvunjika kutokana na kuwepo 
vurugu kubwa baada ya Profesa Lipumba kuingia ndani ya ukumbi huo na 
wafuasi wake wakitaka barua yake ya kutaka kurejea kwenye nafasi yake 
ijadiliwe na kukubaliwa.
KIKOSI CHA TIMU YA TAIFA STARS KITAKACHO SAFIRI KWENDA KUIVAA NIGERIA HIKI HAPA
 
Kocha Mkuu wa timu ya Mpira wa Miguu Tanzania ‘Taifa Stars’, 
Charles Boniface Mkwasa, ametangaza wachezaji 20 watakaounda kikosi 
kitakachosafiri mwishoni mwa mwezi huu kwenda Nigeria kwa ajili ya 
mchezo wa mwisho wa kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya 
Afrika (AFCON 2017) dhidi ya timu ya Taifa ya nchi hiyo, Super Eagles.
Licha ya mchezo huo wa Septemba 3, 2016 kuwa sehemu ya mchuano wa 
kuwania nafasi ya kucheza fainali hizo za AFCON 2017 huko Gabon, lakini 
utakuwa ni wa kukamilisha ratiba baada ya Misri kufuzu kutoka kundi G 
ambalo mbali ya Nigeria na Tanzania, pia ilikuwako Chad ambayo 
iliyojitoa katikati ya mashindano.
“Tanzania hatuwezi kuupuuza mchezo huu, tunaupa umakini kabisa kwa sababu tunacheza ugenini ambako matokeo mazuri 
yanaweza kutusongesha mbele na kuingia ndani ya timu 99 bora katika 
viwango vya FIFA,” amesema Mkwasa.
Katika kikosi chake, Mkwasa ametangaza kutomjumuisha Mshambuliaji wa 
Kimataifa, Thomas Ulimwengu anayecheza klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya
 Kidemokrasia ya Congo (DRC) kutokana na majeruhi ya paja kama ilivyo 
kwa Juma Abdul wa Young Africans ambaye aliumia katika mchezo wa kuwania
 Kombe la Shirikisho dhidi ya Mo Bejaia ya Algeria.
“Timu ilitarajiwa kuingia kambini Agosti 28 siku ya Jumapili, mchezo huo ni wa kukamilisha ratiba ambapo Misri tayari 
wameshafuzu fainali za Afrika,” alisema Mkwasa na kuongeza kuwa kuna 
mchezaji wa Tanzania, Said Carte Mhando anamfuatilia ili ikiwezekana 
baadaye amwite kuchezea timu ya Taifa. Anachezea Klabu ya Brencia Calcio
 ya Italia.
Wachezaji walioitwa:
Makipa; Deogratius Munishi (Young Africans) na Aishi Manula (Azam FC)
Mabeki
Kelvin Yondani (Young Africans),Vicent Andrew (Young Africans)
Mwinyi Haji (Young Africans),Mohamed Hussein (Simba SC)
Shomari Kapombe (Azam FC) na David Mwantika (Azam FC)
Viungo
Himid Mao (Azam FC),Shiza Kichuya (Simba SC),Ibrahim Jeba (Mtibwa Sugar),Jonas Mkude (Simba SC),Muzamiru Yassin (Simba SC),Juma Mahadhi (Young Africans) na Farid Mussa (Tenerif ya Hispania)
Washambuliaji
Simon Msuva (Young Africans),Jamal Mnyate (Simba SC),Ibrahim Ajib (Simba SC),John Bocco (Azam FC) na Mbwana Samatta - CK Genk ya Ubelgiji
Wednesday, August 24, 2016
UVCCM WATARAJI KUFANYA MAANDAMANO YA AMANI AGOSTI 31, 2016 KWA AJILI YA KUELEZA UTENDAJI WA DKT. JOHN POMBE MAGUFULI
Kaimu 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Shaka 
Hamdu Shaka akizungumza na Waandishi wa habari Makao makuu ya Ofisi hizo jijini Dar es Salaam. 
Umoja wa 
Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) wanatarajia kufanya maandamano ya 
Amani Agosti 31 kwa ajili ya kueleza utendaji kazi wa Rais Dk.John Pombe
 Magufuli kwa Watanzania.
Akizungumza
 na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mkuu wa 
Umoja huo, Shaka Hamdu Shaka amesema kuwa maandamano hayo 
wameshamwandikia barua mkuu wa jeshi la Polisi kwa ajili ya kupata 
ulinzi siku hiyo.
Amesema 
kuwa wasipopata ulinzi watafanya kwa kujilinda wenyewe ikiwa ni lengo la
 kufikisha ujumbe kwa wananchi juu ya utendaji kazi wa Rais Dk. John 
Pombe Magufuli.
Shaka amesema kuwa Rais Dk.John Pombe Magufuli amefanya 
watendaji kuwa na utii pamoja na maadili katika utoaji wa huduma kwa 
wananchi.
Aidha 
amesema kuwa maandamano hayo wanaawalika na vijana wa vyama vingine 
kushiriki kwa lengo moja tuu, la kuunga mkono utendaji wa Rais Dkt. John 
Pombe Magufuli.
SAFARI MPYA YA TRENI KUANZA SAFARI ZAKE KWENDA BARA
Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) umeamua kuongeza safari ya tatu ya treni ya abiria ya kawaida kwenda bara ambayo itaondoka Dar es Salaam kila Jumapili, safari ya kwanzai takuwa Jumapili hii ya Septemba 04,2016 saa 9 alasiri.
Taarifa imeainisha kuwa treni hiyo ya huduma ya kawaida itakuwa na mabehewa 12 kutokea Dar es Salaam ikiwa na mabehewa manane ya daraja la 3, mawili daraja la pili kulala na mawili daraja la kwanza. Katika stesheni za Morogoro na Dodoma yataongezwa mabehewa mawili mawili ya daraja la tatu.
Aidha treni ya Deluxe imebadilishwa siku ya kuondoka badala ya Jumapili kwa sasa kuanzia Septemba Mosi, 2016 itakuwa inaondoka siku ya Alhamis saa 2 asubuhi kutoka kituo kikuu cha Dar es Salaam.
Halikadhalika mabadiliko haya pia yataongeza safari za treni ya kwenda Mpanda kutoka Tabora badala ya 2 za sasa zitakuwa 3
kwa wiki ambazo ni Jumatatu, Jumatano na Jumamosi..
Wakati huohuo Uongozi wa TRL umefanya uamuzi wa kihistoria
wa kupeleka huduma za kuuzwa tiketi za safari zake mjini Kasulu ambapo kuanzia Septemba mosi itafungua kituo cha Reli ambacho kitafanya kazi ya kutoa huduma hiyo kwa wasafari wanaotoka Kasulu mjini na maeneo ya jirani .
Kwa uamuzi huo TRL imetoa nafasi za tiketi za  behewa moja la daraja la 3. Pia kuna mpango wa  kufungua kituo kama hicho siku zijazo mjini Kibondo hali itakaporuhusu kulingana na mahitaji halisi ya abiria. 
Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa Niaba ya :
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL,
Nd Focus Makoye Sahani,
Dar es Salaam,
Agosti 23, 2016.
Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa Niaba ya :
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL,
Nd Focus Makoye Sahani,
Dar es Salaam,
Agosti 23, 2016.
Friday, August 5, 2016
WASANII WAWILI WALIOKUWA CHINI YA SHAROBARO RECORDS WAUAWA
 Ude Ude akiwa na swahiba wake Iqu Junior
Kitongoni Tanga
Taarifa kutoka tanga zinaripoti kuwa, wasanii wawili wa mziki wa Bongo fleva ambao walikuwa chini ya lebel ya Sharobaro records UDE UDE na IQU JUNIOR wameuliwa kwa risasi maeneo ya kiwanda cha cement cha Sungura Tanga kwa kosa la ujambazi ambapo walikuwa wanakimbizwa na Polisi.
Report ya Mkuu wa Polisi wa Tanga haijathibitisha tukio hili sio vibaya tukimjua Ude Ude ni nani kwani?,  Huyu alikuwa Msanii na muandishi mzuri wa mashairi ya mziki wa Bongo fleva na amekuwa akiwaandikia wanamuziki maarufu wa Bongo nyimbo ambazo huziimba kwa ufasaha.
Nyimbo alizowahi kuandika ni Single boy ya Ali Kiba, Wangu ya Lady Jaydee featuring Mr. Blue, Lofa ya Top C. Mbali na utunzi pia yeye Ude Ude ni mwanamziki kwani amewahi kutoa wimbo wake uitwao NGOMA INOGILE.
IQU ambae amefunga ndoa miezi michache tu, yeye ni mpiga picha na mwanamuziki pia aliishatoa wimbo aliomshirikisha Ali Kiba uitwao NISAMEHE.
MWENYEKITI WA SIMBA ASHIKILIWA NA POLISI
Evance Aveva
RAIS wa klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Evans Aveva, alikaa rumande kwa siku mbili baada ya kushikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, kutokana
 na amri ya kukamatwa iliyotolewa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na 
Rushwa (Takukuru).
Taarifa za kukamatwa kwa Aveva zilianza kuenea juzi usiku huku kukiwa
 na sintofahamu kubwa juu ya chanzo cha bosi huyo wa klabu kigogo cha 
soka nchini kulala rumande. Hata hivyo, jana vyombo vya dola vilianza kufunguka na kueleza 
masuala mbalimbali yaliyosababisha kushikiliwa kwa Aveva ingawa muda wa 
asubuhi maofisa wa polisi na Takukuru walishindwa kuweka bayana sababu 
hasa ya kumshika bosi huyo. 
Baadaye Takukuru walisema kwamba uchunguzi unaendelea lakini Aveva 
anashikiliwa kwa madai ya matumizi mabaya ya ofisi ingawa Ofisa Habari 
wa Takukuru, Musa Milaba, hakutaka kuweka wazi zaidi.
baadae taarifa za udadisi zikabainisha kuwa kukamatwa kwa Rais huyo ni tuhuma za matumizi mabaya
 ya fedha zilizotokana na mauzo ya mshambuliaji wao Mganda, Emmanuel 
Okwi, aliyeuzwa katika klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia mwaka 2009.
Simba walipokea zaidi ya Sh milioni 600 kutoka kwa klabu ya Etoile baada ya kuuzwa kwa dola 300 za Kimarekani. Inadaiwa kwamba, fedha hizo ziliingizwa kwenye akaunti ya klabu ya 
Simba na baadaye kuhamishwa na kupelekwa katika akaunti ya mtu binafsi 
ambaye ni mwanachama wa klabu hiyo. 
Chanzo: Bingwa
Thursday, August 4, 2016
Wednesday, August 3, 2016
TV 1 KURUSHA MECHI ZOTE ZA LIGI YA UINGEREZA
Kituo cha Televisheni nchini, TV1 leo hii kimezindua kampeni yake inayokwenda kwa jina la Toroka Uje ambayo inawaletea watazamaji wake matangazo ya bure ya mechi zote za Ligi Kuu ya Uingereza maarufu kama English Premier League zitakazoanza kutimua vumbi kuanzia Agosti 13 mwaka huu.
 
Akizungumzia kampeni hiyo Meneja Mkuu wa TV1, Joseph Sayi alisema kuwa Watanzania kwa kipindi kirefu wamekuwa wakitumia pesa nyingi kuangalia ligi hiyo maarufu duniani lakini kupitia TV1 ambayo inapatikana kwenye king’amuzi cha Startimes, Watanzania watakuwa wakitazama mechi hizo bure bila gharama yoyote.
Akizungumzia kampeni hiyo Meneja Mkuu wa TV1, Joseph Sayi alisema kuwa Watanzania kwa kipindi kirefu wamekuwa wakitumia pesa nyingi kuangalia ligi hiyo maarufu duniani lakini kupitia TV1 ambayo inapatikana kwenye king’amuzi cha Startimes, Watanzania watakuwa wakitazama mechi hizo bure bila gharama yoyote.
Naye Meneja Masoko wa TV1, Gillian Rugumamu aliongeza kuwa mbali na watazamaji wa TV1 kufurahia mechi hizo ambazo zitarushwa kuanzia mechi ya kwanza hadi ya mwisho wa ligi, pia wamejiandaa kukutana na watazamaji wa TV1 kupitia michezo mbalimbali, matamasha na mashindano yatakayokuwa na zawadi mbalimbali zikiwemo vifurushi vya king’amuzi cha Startimes na nyingine kibao.
Akizungumzia kuhusu kampeni hiyo ya Toroka Uje, Mkuu wa Uzalishaji vipindi wa TV1, Mukhsin Mambo, alisema kuwa kipindi hicho kitakachoanza kuruka tarehe 10 mwezi huu kitakuwa katika siku tatu ambapo kutakuwa na mijadala ya kandanda, mpira laivu na uchambuzi kuhusu mechi zijazo ambapo uchambuzi huo utaongozwa na wachambuzi wakubwa akiwemo Dr Leaky Abdallah na Ally Kashushu.
Aidha Meneja Masoko wa Startimes, Damien Li aliwahakikisha Watanzania kuwa Startimes haitaongeza bei ya vifurushi wala kutoza chochote kwa watazamaji wa Ligi hiyo kupitia TV1 kwa kuwa ni bure kabisa.
TETESI ZA USAJILI ULAYA
Chelsea wako tayari kumtoa mshambuliaji wa Ufaransa Loic Remy, 29, pamoja na dau litakaloweka rekodi Uingereza kitita cha paundi millioni 65 kwa mshambuliaji wa Everton Romelu Lukaku, 23. (Chanzo Daily Mail)
Everton wamekuwa waking’ang’ania wapewe paundi millioni 75 kwa mchezaji huyo pekee ambaye walimsajili kutoka Chelsea kwa paundi millioni 28 miaka miwili iliyopita. (Chanzo Sun)
Lukaku anafikiria kutoa ombi rasmi ili kulazimisha arudi tena Stamford Bridge. (Chanzo London Evening Standard)
Winga wa Leicester City Riyad Mahrez, 25, amekubali kuhamia Arsenal, hii ni kwa mujibu wa chanzo kimoja kutoka nchini Algeria. (Chanzo Le Buteur)
Kocha wa Manchester City Pep Guardiola anataka kufikia muafaka juu ya dili la paundi millioni 50 la uhamisho wa beki John Stones, ambaye ndiye lengo lake kuu, ingawa Everton wamesisitiza kuwa bado kuna 'gepu kubwa' kati ya klabu hizo mbili juu ya ada ya uhamisho wa mchezaji huyo wa kimataifa wa England. (Chanzo Daily Mirror)
Real Madrid inaweza ikawapa ofa Newcastle ya wachezaji wawili vijana - pengine Mariano Diaz, 23, na Marcos Llorente, 21 – kwa mikopo wa muda mrefu ikiwa ni kama sehemu ya mpango wa kumchukua kiungo wa Ufaransa Moussa Sissoko, 26. (Chanzo Guardian)
Stoke City wanafikiria kumtoa aidha Joselu, 26, Mame Diouf, 28, au Peter Crouch, 35, ikiwa West Bromwich Albion watataka wapewe mchezaji wa kubadilishana kwenye dili la uhamisho wa Saido Berahino, 22. (Chanzo Stoke Sentinel)
Paris St-Germain wamekubali kuwalipa Real Madrid yuro millioni 25 kama ada ya kumsajili winga Jese Rodriguez, 23. (Chanzo Marca)
Bastian Schweinsteiger ameambiwa atapewa nafasi ya kurudi Bayern Munich ikiwa ataondoka Manchester United. (Chanzo Sky Sports)
HUU NDIO USAJILI KAMI LI WA RUVU SHOOTING
Timu ya soka ya Ruvu Shooting, imekamilisha usajili wa wachezaji wake watakaoichezea msimu mpya wa 2016/17.
Wachezaji wapya waliosajiliwa msimu huu, timu walizotoka kwenye mabano ni Jabir Aziz (Mwadui FC),   Richard Peter (Mbeya city), Elias Emanuel (Polisi Morogoro), Clidel Loita (Mji Njombe), Chande Magoja na Fuluzuru Maganga wote kutoka Mgambo JKT, Shaibu Nayopa (Oljoro), Abrahaman Musa (JKT Ruvu) na Renatus Kisasa ambaye ni mchezaji huru.
Aidha wachezaji wazamani walioachwa ni Ally Khan, Yahya Tumbo, Chagu Chagula, Juma Mpakala, Rashid Gumbo, Kulwa Mobi, Gidion Seppo na George Osei.
Timu iko kambini Mabatini ikiendelea na mazoezi ambapo Agost 1, ilicheza mchezo wa kwanza wa kirafiki dhidi ya Mbeya city na kupata ushindi wa bao 1-0, leo Jumatano Agost 3 itakuwa uwanja wa Polisi College, Dar es salaam kucheza na Polisi Dar es salaam ambapo Jumamosi ijayo itakuwa Mabatini ikipambana na Azam fc.
Imetolewa na;
Masau Bwire 
Afisa Habari na mawasiliano Ruvu Shooting.
Tuesday, August 2, 2016
YANGA NAO KUFANYA MKUTANO NA KUCHEZA MECHI YA KUJIPIMA
Baada ya watani wao kufanya mkutano wa mabadiliko nao Young African Sports Club wameitisha mkutano mkubwa tarehe 06 mwezi wa nane. Pamoja na mkutano huo itapigwa mechi kubwa ya kujipima nguvu kati ya Yanga na Mtibwa sugar kutoka turiani manungu Morogoro.
Chini ni taarifa ya mkutano huo.
SIMBA WAMUOMBA MO KUTIMIZA AHADI YAKE
Chini ni barua ya Simba kwenda kwa mkurugenzi wa Mohamed Interprises Kumuoomba asaidie usajili katika kutimiza ahadi yake baada ya wanachama kuridhia mabadiliko.
MAONI YA ZITTO KUHUSU MO SIMBA
Mwanachama wa Simba Zitto Zubery Kabwe nae amejitokeza kwenye mitandao ya kijamii na kutoa maoni yake kuhusu mabadiliko yanayo elekea kufanyika Simba. Hapo chini ni maoni yake kuhusu mgawanyo wa hisa. 
20bn tshs endowment fund for Simba SC ni moja ya pendekezo bora zaidi kutolewa na Mwanamichezo nchini kwetu. Mohamed Dewji anapendekeza kuwa yeye atatoa tshs 20bn na kuziweka kwenye Endowment Fund kisha riba kutumika kuendesha Club. Tutakuwa na club matata sana nchini. Vyuo vikuu vikubwa duniani Kama Harvard vinaendeshwa kwa Mfumo huu anao pendekeza MO. Tukiwa na usimamizi mzuri wa Fedha tutakuwa timu bora kabisa na tutaweza hata kuwa na academy ya Simba Kama ilivyo kwa club kubwa duniani. 
Hata hivyo, nashauri kwenye muundo wa umiliki, mtu mmoja asiwe na Hisa zaidi ya 40%. Ushauri wangu ni mgawanyo ufuatao; 
- Mwekezaji ( MO ) 40% ( mkataba wake wa uwekezaji uonyeshe kuwa kwa kupewa Hisa hizi atafungua endowment fund ya thamani ya tshs 20bn na atakuwa na uhuru wa kuteua trustees wa Fund hiyo. Mwekezaji atakuwa na uhuru wa kuifunga fund iwapo asiporidhishwa na matumizi Fedha zinazotokana na Endowment Fund ). 
-  Wanachama wote wa Simba wagawiwe sawa 40% ( kuwe na cut off ya siku ya mwisho Mwanachama kujiunga kuweza kufaidika na kugawiwa Hisa hizo. Hisa za Simba SC zikishaorodheshwa kwenye soko la Hisa, Mwanachama atakuwa na uhuru wa kuuza Hisa zake freely. 
- 20% ya Hisa ziorodheshwe kwenye Soko la Hisa la Dar Es Salaam kwa ajili ya 1) kuvutia wawekezaji wengine 2) kukuza mtaji wa Kampuni 3) kuwezesha uwazi kwenye uendeshaji wa kampuni kwani Wanachama wote watakuwa wanajua kila kinachoendelea kwenye kampuni na club kwa sababu soko la Hisa Lina ' disclosure rules '. 
Kwanini MO asiwe na 51%? Sio MO tu, Memarts za Simba ziwe wazi kwamba hakuna mtu mmoja au kampuni moja au taasisi yeyote moja itakayoruhusiwa kuwa na zaidi ya 40% ya Hisa za kampuni. Hii itamfanya MO au mwekezaji mwingine yeyote kuhakikisha anatafuta 11% zaidi ili kupitisha maamuzi. Kuna hatari ya kumpa mtu mmoja uwezo wa kufanya maamuzi peke yake. Lazima kumfanya ashawishi japo 11% ya wenye Hisa ili kuboresha maamuzi. Leo ni MO anaipenda Simba, kesho unaweza kuwa na mtu asiye MO. Nadhani 40% ni kiwango cha kutosha kwa Mwekezaji. 
Nashauri wana Simba tusicheleweshe haya MABADILIKO. Tufanye sasa hivi ili msimu huu unaoanza tuwe na timu imara yenye uhakika wa kushiriki Premier League. Mpango wa MO wa Endowment Fund ni Mpango bora na tusipoteze nafasi hii. 
Subscribe to:
Comments (Atom)






 
 
 