Kaimu 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Shaka 
Hamdu Shaka akizungumza na Waandishi wa habari Makao makuu ya Ofisi hizo jijini Dar es Salaam. 
Umoja wa 
Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) wanatarajia kufanya maandamano ya 
Amani Agosti 31 kwa ajili ya kueleza utendaji kazi wa Rais Dk.John Pombe
 Magufuli kwa Watanzania.
Akizungumza
 na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mkuu wa 
Umoja huo, Shaka Hamdu Shaka amesema kuwa maandamano hayo 
wameshamwandikia barua mkuu wa jeshi la Polisi kwa ajili ya kupata 
ulinzi siku hiyo.
Amesema 
kuwa wasipopata ulinzi watafanya kwa kujilinda wenyewe ikiwa ni lengo la
 kufikisha ujumbe kwa wananchi juu ya utendaji kazi wa Rais Dk. John 
Pombe Magufuli.
Shaka amesema kuwa Rais Dk.John Pombe Magufuli amefanya 
watendaji kuwa na utii pamoja na maadili katika utoaji wa huduma kwa 
wananchi.
Aidha 
amesema kuwa maandamano hayo wanaawalika na vijana wa vyama vingine 
kushiriki kwa lengo moja tuu, la kuunga mkono utendaji wa Rais Dkt. John 
Pombe Magufuli.


