
Tuesday, September 30, 2014
Monday, September 29, 2014
MALINDI YALIFUMUA BENCHI LAKE LA UFUNDI BAADA YA KUCHEZA MECHI MBILI TU
| Kocha Abdulghani Msoma na kocha msaidizi Rashid Lato wakiwafatilia kwa karibu vijana wa Malindi. | 
 Klabu  ya  malindi 
ya  mjini  Unguja  imeliongezea  makali 
benchi  lake  la 
ufundi  lililokuwa  likiongozwa 
na  Mohamed  Said 
Shubery  al  maarufu 
Babu  Shube  na  badala 
yake  sasa  litakuwa 
likiongozwa  na  makocha  watatu  na  si
wawili tena  na  wamemuongeza  kocha 
Abdulghani  Himid  Msoma 
katika kuinoa  timu hiyo  inayoshiriki 
ligi  kuu  ya 
Zanzibar  inayofahamika  kama 
Grand malt  premier  league.
Uamuzi  huo  wa  malindi  umekuja  kufuatia 
matokeo  mabaya 
waliyopata  katika  mechi 
zao  mbili  za ligi 
walizocheza  na  mpaka 
sasa  kuwa  hawana 
hata  point  moja  ila  wameambulia 
magoli  mawili  tu  uongozi 
umeamua  kumuongezea  nguvu 
za  kiufundi  kocha 
huyo  mwenye  maneno 
mengi  mfano  wa 
kocha  Chelsea  ya 
Uingereza  Jose  Mourinho, Mohamed  Shubery 
au  Babu. Leo 
asubuhi  alionekana  yuko 
samba samba  na  kocha 
Msoma na  pamoja  na 
msaidizi wake  Rashid  Lato katika mazoezi ya mwisho Katika  uwanja 
wa  Amaan  kabla 
ya  mchezo  wa leo.
 Kocha   Msoma 
aliyeanza  kazi  hiyo 
ya  kuwanoa  Malindi 
juzi  asubuhi  Kwenye 
uwanja  wa  Amaan 
na  jana  kuendelea  na 
mazoezi  hayo  asubuhi 
mtihani wake  wa  kwanza 
ulikuwa   ni  leo  ambapo 
Malindi  ilishuka  dimbani 
kupepetana  na  timu 
ya  Polisi  ya 
Zanzibar  kwenye  uwanja 
wa  Amaan  katika 
mchezo  uliochezwa  saa 
10  Alaasiri  umeshuhudiwa 
Malindi  ikiibuka  na  
ushindi  wa  goli 
moja  kwa  nunge 
dhidi  ya  maafande 
hao  Polisi  Zanzibar, Malindi  sasa 
baada  kuonja  ushindi 
huo  hii  leo 
angalau  sasa  wana 
point  tatu  na 
magoli  matatu.
| .Malindi wakiwa katika mazoezi jana asubuhi ktk uwanja wa Amaan. | 
HUKU NISSAN NYEUSI KULE BMW NYEUPEEE MBONA MNATUCHANGANYA?
Sunday, September 28, 2014
UTURUKI WARUHUSU HIJJAB KWA WANAFUNZI
Nchi ya Uturuki imeondoa marufuku ya kuvaa Hijabu kwa wanafunzi wa shule za Sekondari iliyodumu takribani kwa muda wa muongo mmoja.
Uamuzi huo ulitangazwa siku ya Jumanne na Naibu Waziri Mkuu Bulent Arinc.
Akizungumza na waandishi wa habari Bulent Arinc alisema kwa sasa serikali imeruhusu wanafunzi kuhudhuria shuleni wakiwa wamevaa Hijabu katika shule zote zilizo chini ya Wizara ya
Elimu.
Bulent Arinc ambaye ni msemaji pia wa chama cha Justice and Development (AK) alisema agizo hilo baada ya siku mbili litakuwa lenye kutekelezwa baada ya kupeleka taarifa za kimaandishi katika Wizara husika.
Hijabu ilipigwa marufuku mwaka 1980 kwa wanafunzi, wafanyakazi katika taasisi za umma na serikali muda mfupi baada ya mapinduzi ya kijeshi.
Tangu wakati huo wanawake waliokuwa wakivaa hijabu nchini humo walilazimika kuacha kazi katika ofisi za serikali.
Utawala wa Uturuki umekuwa ukijaribu kuwa mbali na taratibu za kiislamu kwa ajili ya kuridhisha nchi za Ulaya ili kuingizwa katika
umoja wa nchi hizo. Uturuki kwa muda mrefu imetaka kuwa mwanachama wa nchi hizo
za Ulaya bila mafanikio.
umoja wa nchi hizo. Uturuki kwa muda mrefu imetaka kuwa mwanachama wa nchi hizo
za Ulaya bila mafanikio.
Waziri Mkuu ErdoÄŸan aliahidi kuondoa marufuku yote juu ya uvaaji wa Hijabu wakati aliposhinda kwa mara kwanza mwaka 2002.
Tangu wakati huo aliondoa marufuku ya kuvaa Hijabu kwa wanafunzi wa vyuo vikuu. Hata hivyo bado vazi la Hijabu halijaruhusiwa kwa majaji, waendesha mashtaka, maafisa wa kijeshi na wafanyakazi wa kijeshi.
 Cha kuzingatia ni kuwa katika baadhi ya nchi za ulaya ikiwemo uingereza vazi la hijjab linavaliwa na watu wote hata askari kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini.
MATOKEO NA PICHA YA MECHI ZILIZOCHEZWA JANA TANZANIA
Hiyo ni sare ya pili mfululizo kwa kocha Mzambia, Patrick Phiri baada ya wiki iliyopita kutoka 2-2 na Coastal Union Uwanja wa Taifa, licha ya kuongoza 2-0 hadi mapumziko.
Hadi mapumziko, tayari Simba SC ilikuwa inaongoza kwa bao 1-0 lililofungwa na Mganda, Emmanuel Okwi dakika ya 32 akimalizia pasi fupi ya Mohammed Hussein ‘Tshabalala’.
Timu ya Polisi inayofundishwa na Mohammed ‘Adoph’ Rishard ilibadilika na kuanza kusukuma mashambulizi langoni mwa Simba SC ambapo Danny Mrwanda, mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, aliisawazishia Polisi baada ya kumzidi mbio na maarifa beki Joseph Owino kabla ya kumchambua vizuri kipa Hussein Sharrif ‘Cassilas’.
Azam FC imepata ushindi wake wa pili baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting leo kwenye Uwanja wa Chamazi.
Azam FC ambao walianza ligi kwa kuitwanga Polisi Moro kwa mabao 3-1, imeshinda mabao hayo mawili leo, yote yakitupiwa kimiani na Mrundi, Didier Kavumbagu ambaye sasa ana mabao manne.
Azam FC 2 - 0 Ruvu Shooting
Mtibwa Sugar 3 – 1 Ndanda FC
Mbeya City 1 – 0 Coast Union
Mgambo Shooting 0 – 1 Stendi United
Subscribe to:
Comments (Atom)









































-2122405794.jpeg)

