Mabasi ya timu hizo kama yanavyo onekana hapa:
Andrea Pirlo kama anavyo onekana hapo akishuka kwenye ndege:
Friday, June 5, 2015
175 WATHIBITIKA KUFARIKI KATIKA AJALI YA MOTO GHANA



Takriban 
watu 175 wamefariki mpaka sasa kufuatia moto uliotokea katika kituo 
kimoja cha mafuta katika mji mkuu wa Ghana Accra.
Moto huo 
uliozuka siku ya jumatano usiku ulianza wakati wakaazi wa mji huo 
walipokuwa wakikabiliana na siku mbili za mvua kubwa ambayo imewaacha 
raia wengi bila makaazi pamoja na stima.
Mafuriko hayo yaliathiri juhudi za uokozi na huenda yalisababisha moto huo, Tayari Ghana imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo.
Mlipuko 
huo ulitokea hapo jana wakati mamia ya watu walipokuwa wamejihifadhi 
katika kituo hicho cha mafuta kutokana na mvua kubwa zinazonyesha.
Rais wa Ghana, John Mahama amesema janga hilo halitajirudia tena. Bwana Mahama amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mji mkuu, Accra alipotembelea eneo la tukio.
AFISA MMOJA WA FIFA AKIRI KUPOKEA RUSHWA

Wizara ya Sheria ya Marekani imechapisha taarifa inayoelezea jinsi
 Afisa wa zamani wa FIFA Chuck Blazer alivyokiri kuwa yeye pamoja na 
wenzake walipokea rushwa ikiwa ni pamoja na kuichagua Afrika Kusini kuwa 
mwenyeji wa fainali ya kombe la dunia mwaka 2010.
Katika 
taarifa hiyo imeweka wazi mtandao wa malipo ya rushwa ulivyokuwa 
ukifanywa ndani ya shirikisho la soka duniani FIFA, taarifa zinazoegemea
 uchunguzi uliofanywa na shirika la kijasusi la Marekani FBI.
Taarifa 
hiyo ambayo inamwelezea Afisa huyo wa zamani wa Fifa kukiri
 kupokea rushwa sasa huenda ikaibua mengi kwenye kashfa ya rushwa 
inayoindamana shirikisho la FIFA.
Mmerakani
 huyo kwenye taarifa hiyo inadai alikuwa ni mmoja wa watu waliosuka 
mipango ya kupokea rushwa katika tukio jingine la fainali la kombe la 
dunia 1998.
Taarifa 
za Kukiri zipo katika maandishi wakati wa kesi yake mwaka 2013 ilipokuwa akisikilizwa katika mahakama ya Easten New York huko
 Marekani ambapo alikiri makosa kumi yaliyokuwa yanamkabili.
Blazer 
alikuwa afisa wa ngazi ya juu wa FIFA eneo la kanda ya Amerika Kaskazini na
 Kati na ukanda wa nchi Caribbean kuanzia mwaka 1990 hadi mwaka 2011.
Marekani 
imefungua kesi ya rushwa inayowakabili maafisa wa FIFA jambo lililofanya
 Rais wa FIFA Sepp Blatter kuamua kutangaza kujiuzulu.
Subscribe to:
Comments (Atom)






