Young
 Africans Sports Club jana usiku imemuongezea mkataba wa miaka miwili 
mshambuliaji Hamis Friday Kiiza kwa ajili ya kuitumikia klabu hiyo.
 
 Kiiza awali mkataba wake ulimalizika mwishoni mwa mwezi mei mwaka huu 
kabla ya jana kukutana na viongozi wa klabu ya Yanga na kukubaliana 
kuongeza mkataba huo.
 
 Kiiza anakua ni mchezaji wa nne wa 
kimataifa atayeitumikia klabu ya Yanga akiwa pamoja na Didier Kavumbagu,
 Mbuyu Twite na Haruna Niyonzima.
Ni Majemedari
 watatu wa Kamati ya Mashindano ya Yanga SC inayohusika pia na masuala 
ya usajili, Mwenyekiti Abdallah Bin Kleb na Wajumbe wake, Isaac Chanji 
na Mussa Katabaro wamemaliza kazi hiyo usiku huu.
Zoezi
 lilifanya katika eneo la bwawa la kuogelea kwenye hoteli ya Protea, Dar
 es Salaam na Kiiza Jumapili atavaa tena jezi ya Yanga kuichezea kwenye 
mechi ya kirafiki dhidi ya Mtibwa Sugar, Uwanja wa Taifa.  
  | 
| Hamis Friday Kiiza "mabao" |