
Thursday, August 15, 2013
MKURUGENZI WA CRDB KORTINI KWA TUHUMA ZA KUDHALILISHA KIJINSIA
Mkurugenzi wa Benki ya CRDB tawi la Moshi mkoani Kilimanjaro, Francis 
Mollel jana alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi
 kwa tuhuma za kumdhalilisha kijinsia mteja ndani ya benki hiyo, Lulu 
Kajembe.
Mwendesha mashitaka, wakili wa serikali, Patrick Mwita mbele ya Hakimu Swai alieleza kwamba Lulu aliwahi kufanya kazi kwenye benki hiyo na kwamba siku ya tukio Juni 1, 2013, mlalamikaji alikuwa kwenye foleni akisubiri kuhudumiwa ndani ya benki hiyo na ndipo mshitakiwa alimtolea maneno ya udhalilishaji wa kijinsia.
Hata hivyo, mshitakiwa anayetetewa na wakili Kitomo, alikana kosa na mahakama hiyo kumpa dhamana ya shilingi milioni moja na wadhamini wawili wanaotambulika. Mshitakiwa yupo nje kwa dhamana ambapo amezuiwa kusafiri nje ya mkoa na kuwasilisha stakabadhi zote za kusafiria.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi Agosti 21 itakapotajwa. --- (TANZANIA DAIMA)
Mwendesha mashitaka, wakili wa serikali, Patrick Mwita mbele ya Hakimu Swai alieleza kwamba Lulu aliwahi kufanya kazi kwenye benki hiyo na kwamba siku ya tukio Juni 1, 2013, mlalamikaji alikuwa kwenye foleni akisubiri kuhudumiwa ndani ya benki hiyo na ndipo mshitakiwa alimtolea maneno ya udhalilishaji wa kijinsia.
Hata hivyo, mshitakiwa anayetetewa na wakili Kitomo, alikana kosa na mahakama hiyo kumpa dhamana ya shilingi milioni moja na wadhamini wawili wanaotambulika. Mshitakiwa yupo nje kwa dhamana ambapo amezuiwa kusafiri nje ya mkoa na kuwasilisha stakabadhi zote za kusafiria.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi Agosti 21 itakapotajwa. --- (TANZANIA DAIMA)
MUUAJI WA BILIONEA WA ARUSHA AKAMATWA

Polisi wamefanikiwa kumtia mbaroni mfanyabiashara tajiri wa 
madini ya Tanzanite huko Mirerani anayetajwa kuwa ndiye aliyepanga na 
kukodi watu waliomuua bilionea Erasto Msuya. 
Habari za uhakika kutoka ndani ya Jeshi la Polisi 
zimedai kuwa mfanyabiashara huyo alikamatwa mwishoni mwa wiki na jana na
 juzi alikuwa akihojiwa na makachero.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, mfanyabiashara huyo 
ndiye aliyetoa fedha za kununulia pikipiki mbili zilizotumika katika 
mpango huo na pia alitoa fedha kwa ajili ya kununua simu mpya na laini 
mpya.
“Tumewakamata watu wametupa mwanga mzuri na huyo 
mfanyabiashara ndiye aliyetoa fedha za kununulia pikipiki na siku moja 
kabla ya tukio zilihifadhiwa nyumbani kwake,” alidokeza polisi mmoja.
Habari hizo zimedai kuwa polisi pia imewahoji 
mawakala wa kampuni za simu ambao walitumiwa kusajili laini mpya za simu
 zilizotumika kumpigia marehemu na kutumika kupanga mauaji hayo.
Pikipiki hizo mbili, zilinunuliwa siku moja kabla 
ya tukio kisha zikahifadhiwa nyumbani kwa mfanyabiashara huyo hadi siku 
iliyofuata ambapo aliwakabidhi wauaji na zote zimekamatwa.
Mahojiano kati ya mfanyabiashara huyo na Polisi 
yamekuwa yakifanyika kwa siri na katika kituo cha polisi (jina tunalo) 
na kwamba mambo ni mazuri ingawa jina lake halijatajwa.
 
 
Subscribe to:
Comments (Atom)