Friday, August 16, 2013
TRA ILALA YAKAMATA BIDHAA AMBAZO WAFANYABIASHARA WADAIWA KUKWEPA KODI KUPITIA MASHINE ZA EFD
 
Meneja
 Msaidizi wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Mkoa wa Ilala, Catherine Nkelebe 
(kushoto), akizungumza na waandishi wa habari  Dar es Salaam jana , 
kuhusu  TRA mkoa huo kukamata bidhaa mbalimbali za dukani ambazo 
wafanyabiashara wanadaiwa kukwepa kuzilipia kodi kupitia mashine za 
kielektroniki.
 
Marobota ya bidhaa mbalimbali yakiwa TRA Mkoa wa Ilala baada ya kukamatwa.
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), 
Mkoa wa Ilala jijini Dar es Salaam, imekamata bidhaa mbalimbali za 
dukani zenye thamani ya mamilioni ya fedha ambazo wafanyabiashara 
wamefanya hujuma ya kukwepa kulipa kodi kupitia mashine za 
kielektroniki (EFD-Electronic Data Enterchange).
Meneja Msaidi wa TRA Ilala, 
Catherin Nkelebe akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es 
Salaam, alisema bidhaa hizo ambazo ni pamoja na sufuria, Khanga na 
mitumba zilikamatwa kufuatia msako unaoendeshwa na mamlaka hiyo kwa 
kushirikiana na Jeshi la Polisi.
Nkelebe alisema wafanyabishara 
wamekuwa wakitumia mbinu nyingi kuwepa kulipa kodi kwa kukataa kutumia 
mashine maalum za kielektroniki zilizotolewa na TRA kwa kukata 
stakabadhi kwa wateja wanaokwenda kununua bidhaa katika maduka yao.
Alisema ujanja unaofanywa na 
wafanyabiashara ni kwamba mteja akienda kununua bidhaa hususan katika 
maduka ya jumla wanampatia stakabadhi yenye thamani ndogo wakati mzigo 
huo unakuwa na thamani kubwa.
“Unakuta mfano mteja amenunua 
bidhaa za thamani ya shilingi milioni moja lakini mwenye duka anampatia 
stakabadhi mnunuaji yenye thamani ya Sh. 200,000 ili kukwepa kulipa 
kodi,”alisema.
Nkelebe alisema hujuma nyingine 
inayofanywa na wafanyabiashara ni kutoa stakabadhi ambazo hazina maelezo
 yeyote au mchanganuo wa bidhaa zilizonunuliwa kwa lengo la kuiibia 
serikali mapato yake.
Aliongeza kuwa wafanyabishara 
wanafanya ujanja huo kwa hofu ya kwamba iwapo wataandika stakabadhi 
yenye malipo halali watakadiliwa kiwango kikubwa cha kodi  wakati siyo 
kweli kwani TRA haifanya hivyo kwani inamkadiria mtu kodi kulingana na 
biashara yake.
Alisema TRA kwa kushirikiana na 
Jeshi la Polisi wataendelea kufanya msako wa wafanyabiashara wanaofanya 
hujuma hizo na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
NGASSA AHALALISHWA KUCHEZEA YANGA
Kwa mujibu wa Page ya mwandishi maarufu wa habari za michezo ndugu Edo Kumwembe amesema kuwa Mrisho Khalfan Ngassa amehalalishwa kuchezea Yanga na atarudisha hela asilimia hamsini ya gharama za Simba na amefungiwa mechi sita.
Hapo chini ni jinsi Bwana Edo Kumwembe alivyo andika:
CHINI NI HABARI HIYO KUTOKA VYANZO VINGINE:
  
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imepitia usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom na kumuidhinisha Mrisho Ngasa kuchezea timu ya Yanga baada ya kukamilisha usajili wake.
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imepitia usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom na kumuidhinisha Mrisho Ngasa kuchezea timu ya Yanga baada ya kukamilisha usajili wake.
Hata
 hivyo, Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa imebaini 
kuwa Ngasa alisaini mkataba mwingine Simba (katika kipindi ambacho 
alikuwa na mkataba na Azam) ambapo anatakiwa kurejesha fedha alizopokea 
(sh. milioni 30) pamoja na fidia ya asilimia 50 (sh. milioni 15) ya 
fedha hizo kwa Simba.
Kamati
 pia imemfungia mechi sita za mashindano (kuanzia mechi ya Ngao ya 
Jamii), na anatakiwa awe amelipa fedha hizo ndani ya kipindi hicho cha 
kukosa mechi hizo. Akishindwa, hataruhusiwa kucheza hadi atakapolipa 
fedha hizo.
Vilevile
 Kamati imepitia pingamizi zote zilizowasilishwa kuhusu usajili wa 
wachezaji, kukatiza mikataba ya wachezaji na kuzitaka klabu husika ziwe 
zimetatua masuala hayo hadi Alhamisi (Agosti 22 mwaka huu).
Kwa
 upande wa wachezaji wa kigeni, Kamati imeagiza wasiruhusiwe kucheza 
hadi watakapopata Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC) pamoja na vibali 
vya kufanya kazi nchini (work permits).
Kamati
 hiyo itakutana tena Ijumaa (Agosti 23 mwaka huu) ili kupata ripoti za 
pingamizi ilizoagiza ziwe zimefanyiwa kazi hadi Agosti 22 mwaka huu na 
kutoa uamuzi kwa pande ambazo hazikuafikiana.
WABUNGE 11 WANASURIKA KIFO BAADA YA BASI WALILO PANDA KUTAKA KUUNGUA

Wakati 
msafara wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ukielekea Wilayani 
Missenyi kukagua sehemu utakapojengwa uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa 
Omukajunguti, gari aina ya Costa lenye namba za usajili T 570 BYU 
lilowabeba Waheshimiwa Wabunge 11 lilipata hitilafu na kutaka kuungua.

Ajali 
hiyo ilitokea eneo la Mwanzo Mgumu kilometa moja kutoka mpakani mwa 
Wilaya ya Bukoba na Wilaya ya Missenyi ambapo gari hilo aina ya costa 
lilianza kutoa moshi mwingi kwa upande wa nyuma wakati likiwa kwenye 
mwendo mkali na kuleta hofu kubwa kwa abiria walikuwemo ndani ya gari 
hilo.
Mara baada ya dereva kugundua kuwa 
gari analoendesha linataka kuungua alilisimamisha na kuwaambia abiria 
wake kuwa gari linaungua.
Kwa 
mujibu wa wabunge waliokuwemo kwenye gari hilo, baada ya kuambiwa kuwa 
gari linaungua kila mmoja alifanya juhudi za kujiokoa, wengine wakipitia
 madirishani.
Kwa Bahati hakuna Mbunge aliyeumia isipokuwa Mhe. Batenga aliumia mkono kidogo baada ya kubanana sana mlangoni.
Baada ya kila mmoja kutoka gari hilo liliendelea kutoa moshi mzito sana lakini kwa halikushika moto na baadae lilizimika na kuacha kutoa moshi.
Baada ya kila mmoja kutoka gari hilo liliendelea kutoa moshi mzito sana lakini kwa halikushika moto na baadae lilizimika na kuacha kutoa moshi.

Wabunge 
waliokuwemo katika gari hilo ni Rebbecca Mngondo (Arusha Viti Maalumu), 
Rita Kabati (Iringa Viti Maalumu), Mariam Msabaha (Zanzibar Viti 
Maalumu), Mhe. Batenga (Kagera Viti Maalumu), Mhe. Madabida (Dar es 
Salaam Viti Maalum), Clara Mwatuka (Mtwara Viti Maalumu).
Wengine ni Mzee Hussein (Zanzibar), 
Mussa Haji Kombo (Pemba Zanzibar), Abdul Mteketa (Jimbo la Kilombelo), 
Mutula Mutula (Jimbo la Tunduru Kusini).
Aidha Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Peter Serukamba Hakuwemo katika gari hilo lilotaka kuungua.
Aidha Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Peter Serukamba Hakuwemo katika gari hilo lilotaka kuungua.
SHEIKH PONDA APELEKWA GEREZANI SEGEREA
Leo
 hii, Sheikh Ponda Issa Ponda (54) aliyekuwa amelazwa katika wodi ya 
Kitengo cha Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu 
(MOI) alikokuwa akipatiwa matibabu, amehamishiwa katika gereza la 
Segerea.Sheikh Ponda bado anauguza majeraha yake ya mkono aliyoyapata huko Morogoro ila jeshi limemchukua na kumpeleka Segerea akamalizie kuuguza majereha huko huko Segerea.
Kwa mujibu wa mashtaka aliyosomewa akiwa MOI, Sheikh Ponda atalazimika kurudishwa tena mahakamani siku kesi yake itakapotajwa Agosti 28 mwaka huu, ambapo upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Kwa mujibu wa mashtaka aliyosomewa akiwa MOI, Sheikh Ponda atalazimika kurudishwa tena mahakamani siku kesi yake itakapotajwa Agosti 28 mwaka huu, ambapo upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
VIDEO: KIJANA AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAAM
Siku moja baada ya ziara ya kushtukiza ya waziri wa uchukuzi Dk. Harison
 Mwakyembe, kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini
 Dar-es-Salaam, kiasi kikubwa cha dawa za kulevya kimekamatwa uwanjani 
hapo katika harakati za kusafirishwa kwenda nchi za nje.
Chuma Kikikatwa ili kutoa Heroin iliyofichwa ndani yake.
Heroin ikionekana baada ya Chuma kukatwa kama unavyoona hapo pichani.
Subscribe to:
Comments (Atom)






