CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 14 MACHI, 2013
Ndugu waandishi wa habari,
Tumewaita
 hapa leo, ili kupitia kwenu tuweze kutoa taarifa inayohusu kukamatwa 
kwa mmoja wa viongozi wa chama chetu, Wilfred Lwakatare, Mkurugenzi wa 
Ulinzi na Usalama, aliyekamatwa jana tarehe 13 Machi 2013, ofisini kwake
 makao makuu ya CHADEMA.
Jeshi la polisi linasema limemkamata 
Lwakatare likimtuhumu kuhusika na mashambulio ya watu mbalimbali 
kutokana na ushahidi uliopo kwenye walioita, viedo ambayo pia 
imesambazwa kwenye mitandao ya kijamii.
Kwanza, tunapenda 
kuwaambia umma wa watanzania na watu wote duniani kwamba, CHADEMA hakina
 nia yoyote ya kuzuia polisi kutenda kazi zake, iwapo watakuwa wanafanya
 hivyo kwa mujibu wa sheria.
Bali, tunachoeleza hapa ni jinsi 
polisi na vyombo vingine vya dola vinavyoshiriki katika kutengeneza 
paropaganda chafu dhidi ya CHADEMA za kuwahusisha viongozi wa CHADEMA na
 unyama unaoendelea nchini wa kutesa watu, kupiga, kung’oa kucha na 
baadaye kuwatekeleza wakiwa nusu mfu.
Mpango huu ulianza katika 
tukio la kutekwa kwa Dk. Steven Ulimboka, ukaenda kwa Mwandishi wa 
habari, Daudi Mwangosi na baadaye kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri 
Absalom Kibanda; na kwa bahati mbaya sana, kwa namna moja au nyingine, 
mkakati huu umekuwa ukilihusisha jeshi la polisi katika hatua za 
utekelezaji wake.
Kuweka kumbukumbu sawa, tunaweza kurejea suala 
la kuuawa kinyama kwa Mwangosi, unyama uliosimamiwa na kufanikishwa 
chini ya uangalizi wa kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Michael 
Kamuhanda.
Mara baada ya tukio hilo, jeshi jeshi la polisi 
kupitia kamishana wake, Paul Chagonja lilitoa kauli kuwa Mwangosi 
alilipuliwa na kitu alipokuwa anawakimbilia polisi kujisalimisha 
akitokea kwa wafuasi wa CHADEMA, jambo ambalo limethibitika kuwa 
halikuwa na ukweli hata kidogo.
Mpaka sasa, jeshi la Polisi halijamchukulia hatua zozote za kisheria Kamhanda aliyesimamia na kufanikisha kifo cha 
 
 
Mwangosi, pamoja na ushahidi wa kuhusika kwake kuwepo wazi.
Aidha,
 pamoja na ukweli uliobainishwa na tume zote zilizotumwa kuchunguza 
suala la Nyororo Iringa, kusema Polisi walivunja sheria, walitumia nguvu
 isiyohitajika, bado mpaka leo hii wanachama 42 wa CHADEMA wanashikiliwa
 na polisi mkoani Iringa kuhusika na vurugu za Nyololo, Mufindi, Iringa.
 Waandishi mtakumbuka kuwa Taarifa ya Kamati ya Nchimbi ilitofautiana 
kabisa na Taarifa ya Tume ya Haki za Binadamu nay a MCT. Baada ya kazi 
ya Tume na Kamati hizo hakuna Taarifa hata mmoja imetolewa na Polisi, 
walsa hakuna watu waliohojiwa tena ukiaachawaliokamatwa kabla ya Taarifa
 za Tume hizo. Wala sijaona kwa bahati mbaya vyombo vya habari 
vikichambua Taaarifa hizo kwa kina,
Katika nyakati mbalimbali, 
CHADEMA tumefungua jalada Polisi, na nyingine amezifungua Mhe. 
Lwaklatare mwenyewe akilalamikia mchezo mchafu tunaofanyiwa ikiwa ni 
barua kuandikwa kwa majina yetu, yenye sura ya kutuchafua. Mojawaopo 
ikidhaniwa kuandikwa na Rwakatare mwenyewe akiomba Tshs 200 millioni kwa
 ajili ya vijana anaodhaniwa kuwaleta toka Tarime kwa ajili ya Igunga. 
Hadi leo Polisi hawajamhoji Lwakatare mwenyewe, wala hatujasikia 
upepelezi wowte ukifanyika.
Aidha tulitoa Taarifa ya mtu 
aliyepewa bunduki wakati wa uchaguzi wa Igunga akituhumu kuwa amepewa 
bastola hiyo kwa lengo la kudhuru wakati wa Kampeni ya Igunga. Tumetoa 
mpaka nay a Bastola husika na mahali ilipotengenezwa. Polisi hadi leo 
hawajatoa Tamko lolote kama Bastola hiyo iliyotengenezwa China 
imesajiliwa kwa jina la nani, na hivi sasa ipo kwa nani. Lakini kwa 
tukio tu la Lwakatare na picha yake kubandikwa kwenye Mtandao, Polisi 
tayari wameisha kumkamata. Ni dhahiri kuna mchezo unachezwa dhidi ya 
CHADEMA, na Polisi kuiingizwa au kwa kujua au kutokujua katika mtego 
huo.
Sasa hapo mnaweza kujiuliza, hapo haki ipo wapi? Yaani 
waliotajwa na tume yaani polisi – wapo huru, lakini wanaCHADEMA 42 ambao
 hawakutajwa popote na tume wanasota gerezani.
Hata katika suala 
la Dk. Ulimboka, jeshi la Polisi halikutelekeza wajibu wake kikamilifu. 
Jeshi hilo limekataa kumhoji Dk. Ulimboka na wala kuwahoji baadhi ya 
watuhumiwa wakuu wanaotajwa kuhusika moja kwa moja katika kumteka Dk. 
Ulimboka, akiwemo Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Jack Zoka, Afisa
 wake Ramadhani Ighondo mwengine anayeitwa Nzowa.
Vilevile, kwenye 
tukio la kutekwa kwa Kibanda, ambalo linafanana kwa kiasi kikubwa na 
lile la Dk. Ulimboka, Afisa Mtendaji Mkuu wa New Habari Corporation, 
Hussein Bashe, ametaja kuhusika kwa polisi katika utekaji wa Absalom 
Kibanda, na baadaye akamtaja Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa 
Kimataifa, Bernard Membe, lakini mpaka sasa, jeshi la Polisi 
halijachukua hatua zozote ama kwa waliotajwa au kwa aliyetaja.
Lakini
 katika hili la Lwakatare CHADEMA kilipata taarifa mapema kuwa upo 
mkakati unaoratibiwa na kufanikishwa na Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa 
Taifa, Jack Zoka na genge lake lenye wajumbe mashuhuri, Ramadhani 
Ighondo na Nzowa linalotaka kukihusisha CHADEMA na njama za kumdhuru 
Kibanda ili kukidhoofisha kisiasa. Lilipotokea hili la Lwakatare 
tukasema, sasa kile tulichoambiwa ndiyo hicho kimekuja.
Bahati 
njema gazeti la Mwananchi la leo linasema Lwakatare anatuhumiwa kupanga 
njama za kumdhuru Mhariri wa gazeti hilo, Denis Msacky, na kwamba 
Lwakatare amekamatwa baada ya kuonekana kwenye video iliyosambazwa 
kwenye mitandao ya kijamii haraka inayomuonyesha Lwakatare akipanga 
njama hizo hatujui baadhi ya taarifa zingine ingwa kwa hiki kilichopo 
kwenye mtandao hakuna popote alipotajwa Msaky. Si nia yangu kuingilia 
upelelezi wa Polisi, lakini nimesema CHADEMA tumefurahi kwa kuwa iwapo 
kwa utaratibu huu au wowote ule fursa itapatikana na ukweli wote 
kutolewa hadharani. Ni imani yangu kuwa zoezi hili litafuata sheria na 
taratibu zote zilizokwa na Katiba yetu kulinda haki za mtu.
Sasa kutajwa kwa Msacky inawezekana hilo la Kibanda halijaiva, au pengine liko njiani; ama wameona aibu kuliingiza kwa sasa.
Lakini
 Waandishi wa Habari, mnajua kuwa mara baada ya Kibanda kutekwa, 
Ridhiwani Kikwete na Nape Nnauye walivyoshangilia kutekwa kwa Kibanda 
katika mtandao huo huo uliotumika kumkamata Lwakatare bila kuwakamata 
wahusika hao ambao waliingia kwenye mtandao kwa ID yao wenyewe. 
Akiandika katika mtandao wake wa face book Ridhiwani alisema: “Na hili 
la Kibanda mtasema ni kazi ya Ramadhani Ighondo, afisa usalama pale 
Ikulu?”
Kwanza, kauli hii ya Ridhiwani ilikuwa inathibitisha 
kwamba aliyepanga njama za kumteka Dk. Ulimboka, ni Ramadhani Ighondo wa
 Ikulu.
Pili, Ridhiwani alikuwa anataka kuaminisha jamii kwamba 
katika hili la Kibanda, yeye na kundi lake hawahusiki, bali wanaohusika 
ni CHADEMA; hivyo akawa anachokoza mjadala ambao ulishapangwa ili 
baadaye vyombo vya dola viweze kuuchukua, na hivyo ndivyo ilivyotokea.
Tunazo
 taarifa kutoka vianzio vyetu vya ukakika ndani ya Usalama wa Taifa kuwa
 baada ya Ridhiwani kuweka andishi lake kwenye facebook, aliingia kiwewe
 sana hasa baada ya Hussein Bashe kuja juu. Ridhiwani anafahamu nguvu ya
 Bashe kwenye kufuatilia suala la kutekwa kwa Kibanda na hivyo amemuomba
 baba yake kuvitumia vyombo vya dola kumuokoa. CHADEMA haijawa na 
haitakuwa, lakini tuliyoambiwa yametimia, na mengine zaidi yanakuja, 
kwani kwa Taarifa zetu hiyo yaliyotokea “ni cha mtoto”. Na wala hatutaki
 kutabiri mbinu zitakazotumika kumwokoa.
Ndugu waandishi wa 
habari; katika mlolongo wa kuwakamata viongozi wa CHADEMA, yumo Mbunge 
wa Iringa, Mchungaji Msigwa. Mheshimiwa Msigwa tunaambiwa na watu wetu 
wamemtafuta kwa muda mrefu sasa. Wanasema sumu anazotema bungeni na 
kwengineko dhidi ya idara ya usalama ya taifa juu ya tuhuma za 
kuhusishwa na wizi wa nyara za serikali, zinawanyima usingizi na hivyo 
wanataka wamnyamazishe.
Wanataka kujua kutoka kwa Msigwa ni nani
 aliyevujisha na kumpa taarifa zile za ujangiri wa wanyama pori 
zinazohusisha CCM, usalama wa taifa, polisi na Jeshi la Wananchi wa 
Tanzania (JWTZ). Msigwa anaonekana kuwa ni jasiri kusemea udhaifu wa 
idara ya usalama, wanaamini anavyo vitu vingi na wao wangependa wajue 
ana nini na anapewa na nani.
Tayari Mchungaji Msigwa ameondolewa
 kwenye kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira na kupelekwa 
Kamati ya Kilimo ili kulinda uchafu wa serikali, wakati yeye ni waziri 
kivuli wa Maliasili na Utalii na Waziri kivuli anatakiwa kuwa Kwenye 
Wizara ya Sekta anayoisemea, na wala hajaomba Wizara ya Kilimo.`ni 
dhahiri syndicate ya mfumo huu wa kutaka kuisambaratisha CHADEMA. 
Huhitaji kwenda chuo Kikuu chochote, kuelewa hili.
CHADEMA 
kinafahamu kwa undani, kwamba uzushi huu wa Tape ya “Bukoba Boy”.Tunajua
 huu umeanzishwa na kuhusisha Usalama wa Taifa, akiwemo Ighondo na 
wenziwe pale Ada Estate. Huyu Ighondo ambaye anafahamika pia kwa jina la
 “Rama” tunamfahamu vizuri sana. Aliwahi kufanya kazi ya katibu wa 
UV-CCM wilaya ya Singida Vijijini, kati ya mwaka 2006 na 2008 na ndiye 
aliyekuwa akitumia simu na 0713760473 katika mawawsiliano yake na Dr. 
Ulimboka kwa simu na 0713731610 mpaka takriban dakika 3 kabla ya 
Ulimboka kutekwa. Gazeti la Mwanahalisi liliandika taarifa ya uchunguzi 
ya kina ya Jambo hilo.
Rais wetu amenukuliwa na magazeti ya 
Serikali Addis Ababa akisema kuwa Mwanahalisi ilifungiwa kwa sababu ya 
‘kuchochea uasi katika majeshi yetu’ au maneno Kama hayo. Sitaki kumwita
 Rais wetu wwongo leo lakini kwa kuwa Taarifa hiyo haijakanushwa wala na
 Rais, wala na Ikulu, tunaamini maneno hayo ni kweli ametamka. Tunamtaka
 Rais Kikwete atamke maneno hayo hayo hapa nchini. Kwa njia yeyote ili 
ili Watanzana wengi na hasa wasomaji wa Mwanahalisi, na hata majeshi 
yetu amba kimsingi ninafahamu walilipenda Gazeti la Mwanahalisi wamsikie
 kwa masikio yao wenyewe. Taifa linawekwa pabaya sana Rais anapofikia 
kutoa matamko ya upotoshwaji mkubwa kiasi hicho tena nje ya nchi.
Ndiyo
 maana tunaposema Idara ya Usalama wa Taifa, ni tawi la CCM, 
tunaushahidi. Kwa mfano, tunajua jinsi baadhi ya watendaji wajuu wa 
idara hiyo kama vile, Zoka na vibaraka wake wadogo akiwamo Ighondo, ni 
radical wa CCM, wenye ushabiki uliopitiliza.
Hata ukiangalia 
jinsi walivyotekeleza mpango wa utekaji wa Dk. Ulimboka, kwamba 
walifanya hivyo mbele ya macho ya Dk. Deogratias Michael, haraka 
utabaini kuwa utekaji huu ulifanywa kwa ushabiki wa kulinda CCM.
Ndugu
 waandishi wa habari, kutokana na yote hayo hayo sasa tunasema 
ifuatavyo: Kwamba jeshi la polisi lifanye kazi yake bila ushabiki wa 
kisiasa au shinikizo la wanasiasa.
Ndugu Waandishi,CHADEMA haiko 
tayari kuruhusu watu wenye maslahi binafsi kutuchafua mbele ya jamii. 
Katika hilo, tutapambana na yoyote bila kujali cheo chake, madaraka yake
 serikalini, fedha alizonazo au madaraka mengine.
Wakati polisi 
wakitekeleza hilo, tunamtaka Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi,
 ajitokoze hadharani kueleza umma juu ya mgogoro wake na Kibanda. 
Tunavyofahamu sisi, Kibanda aliteuliwa kuwa mjumbe katika kamati ya 
kubuni vazi la taifa. Lakini alijitoa na kusema aliyemteuwa yaani - 
Nchimbi - ambaye wakati huo, alikuwa waziri wa habari, utamaduni na 
michezo, ndiye aliyeshinikiza polisi kumfungulia kesi ya uchochezi 
mahakamani.
Hadi sasa hatujapata taarifa za wazi zinazoonyesha 
kama uadui wa wawili hawa uliisha, na kwamba Nchimbi sasa ndiye waziri 
wa mambo ya ndani, ambapo polisi wanawajibika kwake. Tuna mashaka kuwa 
uchunguzi wa tukio lililomkuta Kibanda unaweza kudhoofika.
Kutokana na hayo yote CHADEMA tunasema nini sasa:-
i)
 CHADEMA katika hatua hii ya awali, tunafuatilia kwa karibu sakata lote 
la ukamataji wa Lwakatare na kuona kama sheria za nchi, taratibu 
mbalimbali na misingi ya Haki za Binadamu inafuatwa kuikamilifu.
ii)
 Tunarudia tena madai yaliyotolewa mara nyingi na CHADEMA, kwa Rais 
kuandikiwa barua na Mwenyekiti wetu, Iundwe Judicial Commission of 
Inquiry (Tume Huru ya Kimahakama kuchunguza vifo vyote vyenye utata na 
sura ya kisiasa). Serikali inaogopa nini kuunda Tume hii huru ili ukweli
 Ujulikane? Iweje CHADEMA inayotuhumiwa Kupanga njama wanaishinikiza 
Serikali kuunda Chombo huru na Serikali ndiyo inayopata kigugumizi?
iii)
 Kwa wale walioumizwa na kujeruhiwa kama kina Ulimboka Kibanda na 
wengine, tunarudia Tamko letu la kuwa hatuna Imani na uchunguzi 
unaofanywa na Jeshi la Polisi kwa kuwa viongozi wa Jeshi hilo ni sehemu 
ya watu tunaowatuhumu kwa kuhusika kwa njia mbalimbali, na Ushihidi wa 
wazi na Taarifa mbili za Serikali kupingana yaani Taarifa ya Kamati yqa 
Nchimbi na Tume ya Haki za Binadamu. Tutaiaminije Polisi na Serikali kwa
 Taarifa ya Kamati ya Nchimbi? Mwendawazimu tu anaweza kuwa na imani 
baada ya Taartifa zile 3.
iv) Kuokana na upotoshwaji mkubwa, na 
kutokana na uhakika tulionao mkubwa Mwanahalisi ilifungiwa si kwa sababu
 yeyote ile, bali kutoka na kukomalia swala la Dr Uliomboka na hasa 
uhusika wa Ighondu, Afisa Usalama anayefanya kazi Ikulu chini ya Raisi 
mwenyewe. CHADEMA sasa tunaitaka rasmi Serikali ifungulie Gazeti nla 
Mwanahali kwa sababu hatuwezi kuendelea kuvumilia uikandamizaji huu wa 
uhuru wa Habari, ambao sasa unaelekea kuota mizizi nchini kwetu. Na 
kweli ninawaomba na kuwataka waandishi wote msimame imara, bila kujadili
 itikadi, au tofauti zetu zozote zile na kusimamia uhuru wa Habari. 
Tunataka vivyo hivyo, kwa wanaharakati mbalimbali. Waache hofu, eti 
wanaogopa kuhusishwa na vyama vya Siasa! Haki ni haki na haina rangi ya 
bendera ya chama chochote.
Ndugu Waandishi Nawashukuru sana
Imetolewa Makao Makuu ya CHADEMA, na,
Dr. Willibrod P. Slaa
KATIBU MKUU - CHADEMA