Wednesday, July 24, 2013
GONZALO HIGUAIN NA PEPE REINA WANAFANYA VIPIMO VYA AFYA NAPOLI SASA HIVI

Inaonekana Arsenal imepoteza nafasi ya kumsajili mshambuliaji wa kiargentina Gonzalo Higuain ambaye imemuwania kwa muda mrefu baada ya mshambuliaji kukaribia kujiunga na klabu ya Napoli ya Italia.
Kwa mujibu wa mtandao wa Sky News ni kwamba hivi sasa nchini Italia mshambuliaji Gonzalo Higuain na kipa wa Liverpool Pepe Reina ambaye nae alihusishwa na Arsenal huko nyuma wapo kwenye vipimo vya afya vya kujiunga na klabu ya Napoli.
Kwa mujibu wa mtandao wa Sky News ni kwamba hivi sasa nchini Italia mshambuliaji Gonzalo Higuain na kipa wa Liverpool Pepe Reina ambaye nae alihusishwa na Arsenal huko nyuma wapo kwenye vipimo vya afya vya kujiunga na klabu ya Napoli.

Real 
Madrid na Napoli zimekubalina ada ya uhamisho wa Higuain kuwa kiasi cha 
£32million na kukubaliana na mchezaji mwenyewe mkataba wa miaka mitano 
kwa mshahara wa paundi 140,000 kwa wiki.
AZAM FC KUFANYA ZIARA KAMA YA MANCHESTER CITY
 
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Wana 
lambalamba Azam fc wanatarajiwa kuondoka  Agosti 2 mwaka huu kuelekea 
nchini Afrika kusini kwa ajili ya kuweka kambi ya kujiandaa na michuano 
ya ligi kuu soka Tanzania bara na michuano ya kimataifa mwakani ambapo 
watakaa kwa wiki mbili.
Afisa
 habari wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga amesema wameamua kufanya ziara 
bondeni kwani wao wameendelea zaidi kisoka kwa maana ya kuwa na ligi 
bora, timu bora na mfumo wa kisasa wa kuendesha soka, hivyo watajifunza 
mambo mengi kutoka kwao.
Jafar
 alisema ziara hiyo itakuwa na manufaa makubwa sana kwani watacheza na 
klabu kubwa za huko wakiwemo Supersport United na Orland Pirates.
“Malengo
 yetu ni kufanya makubwa katika michuano ya kimataifa, lakini Ubingwa wa
 ligi kuu ni muhimu sana kwetu. Na ndio maana tunaenda Afrika kusini 
kuweka kambi ya wiki mbili”. Alisema Jafar.
Kuhusu
 usajili, Jafar alisema wao hawajasajili mchezaji yeyote mpaka sasa na 
hawana mpango wa kufanya hivyo kwani kikosi chao kipo kamili gado.
“Timu
 yetu ni nzuri sana, kusajili mara kwa mara kunaharibu timu, sisi tuna 
wachezaji wengi wakiwemo vijana wetu na ndio maana hatuhangaiki na 
usajili”. Alisema Jafar.
Wakati
 huo huo shirikisho la soka Tanzania, TFF, limethibitsha kupokea barua 
kutoka klabu ya Azam fc kuwa wanatarajia kuondoka nchini kuelekea Afrika
 kusini.
Katibu mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema Azam wamefanya vziuri kuwataarifu wao ili waende kwa kibali sahihi.
Subscribe to:
Comments (Atom)

