
Thursday, June 6, 2013
MAREKANI WAANDAA SHERIA ITAKAYO KATAZA WATU KUVAA MLEGEZO

Sina 
shaka umeshasikia style za uvaaji wa suruali hususan kwa wanaume zenye 
majina kama mlegezo au kata k, au yawezekana ukawa huzijui kwa majina 
lakini umeshashuhudia vijana wamevaa suruali chini ya makalio.
Kama 
ambavyo mabinti wamekuwa wakilaumiwa kwa mavazi ya kuonyesha miili yao 
hasa sehemu nyeti, na upande wa wanaume wamekuwa wakilalamikiwa kwa 
style hiyo ya uvaaji ambayo imeonekana kuigwa hata na vijana wadogo 
ambao bado wako shuleni.
Katika hali 
ya kukerwa na tabia ya vijana kuvaa suruali chini ya makalio uongozi wa 
Wildwood, New Jersey nchini Marekani umeandaa sheria mpya itakayoweza 
kuwadhibiti wale wote wenye tabia hiyo ya kuvaa mlegezo na kukatiza 
mitaani.

Sheria 
hiyo inaelekeza wavaaji wote wa suruali, kaptura, mavazi ya kuogelea na 
sketi zisivaliwe chini ya inchi 3 kutoka kiunoni mwa mvaaji.
Mayor wa 
Wildwood Ernie Troiano Jr. aliwaambia waandishi wa habari kuwa 
amechoshwa na malalamiko anayoyapata juu ya vijana wanaotembea makalio 
nje kwa kushusha suruali zao kupita kiasi.
HII NDIO KAULI YA M 2 THE P BAADA YA KUFIKA TANZANIA KUMZIKA MANGWEA
 
 Rafiki wa wa karibu wa marehemu Albert Mangwea aliyekuwa amelazwa nchini
 Afrika Kusini amerejea Tanzania na yuko njiani akielekea mkoani 
Morogoro kwaajili ya kushiriki mazishi ya swahiba wake Mangwea jioni ya 
leo (June 6).Akizungumza na Times Fm asubuhi hii Mgaza Pende a.k.a M 2 
The P amewashukuru watanzania kwa kumuombea japo hali yake bado haijawa 
nzuri sana lakini ameamua kurudi Tanzania kuja kumzika ndugu yake 
Mangwea. “Ndugu zangu watanzania mimi ni Mgaza Pende M 2 The P 
nawashukuru sana kwa kuniombea mpaka muda huu, nimeweza kuwasili 
Tanzania salama na tutakuwa pamoja kwenda kumzika ndugu yangu kipenzi 
changu Albert Mangwea, nawashukuru sana watanzania kwa kuniombea 
asanteni na endeleeni kuniombea hali yangu bado haijawa nzuri zaidi, 
asanteni,” alisema. Msikilize hapa 
PICHA ZA UTOAJI WA HESHIMA ZA MWISHO KWA MAREHEMU MANGWEA MOROGORO
Meza kuu 
hii ikiwa ni maandalia ya kuuwaga mwili wa msanii marehemu Albert 
Mangwea aliyefariki dunia na anatarajiwa kuzikwa leo mkoani 
morogoro.Utaratibu huu umeandaliwa katika uwanja wa jamuhuri mkoani 
morogoro kwa lengo la kuwapa fursa wakazi wa mji huo kupata nafasi za 
kuuwaga mwili huo kabla ya maziko
Umati 
mkubwa wa wakazi wa morogoro waliojitokeza katika zozi za kuwaga mwili 
wa msanii huyo mchana huu kabla ya maziko yake leo.Marehemu albert mangwea alifariki wiki 
iliyopita nchini afrika kusini na maziko yake yatafanyika leo mkoani 
hapa.

 Mama Mzazi wa Mangweha, Denisia Mangweha akiwa nyumbani kwake kabla ya safari kuelekea Uwanja wa Jamhuri.

Mkuu
 wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera asubuhi hii amefika nyumbani kwa Mama
 Mangwea eneo la Kihonda Mazimbu Road na kumpa pole kwa niaba ya wakazi 
wote wa mkoa wa Morogoro. Baada ya kutoa pole, Mhe. Bendera aliongoza 
umati wa watu kutoka Kihonda kuelekea Uwanja wa Jamhuri kwa shughuli za 
kuaga mwili wa Albert Mangwea aliyefariki dunia Mei 28 mwaka huu nchini 
Afrika Kusini. Mangwea anatarajiwa kuzikwa katika makaburi ya Kihonda 
nje ya Kanisa la Mtakatifu Monica jirani kabisa na alipozikwa baba yake 
mzazi Mzee Keneth Mangwea.
MAJANGA YAZIDI MUANDAMA MR. NICE SASA MKATABA WAKE NA GRAND PA RECORDS YA KENYA WAVUNJWA
Mwanamuziki aliyevumbua staili ya muziki ya TAKEU (Tanzania Kenya Uganda), Mtanzania Lukas Mkenda aka Mr Nice amepoteza mkataba wake na kampuni ya kurekodi muziki ya nchini Kenya, kwa kile kilichoelezwa na kampuni hiyo kuwa ni tabia ya Mr Nice ya uvivu, ulevi, asiyeaminika na asiye na ushirikiano. 
Zaidi ya maandishi yaliyoandikwa na GrandPa Records kwenye ukurasa wao wa Facebook, pia wamezungumzia suala hilo walipohojiwa na kituo cha EA Radio ambapo wamesema Mr Nice amesema ataendelea kubaki mjini Nairobi nchini Kenya akitafuta kujiweka sawa. 
Subscribe to:
Comments (Atom)



