Facebook Comments Box

Sunday, September 28, 2014

COUTINHO NA TEGETE FITI KUWAVAA PRISONS LEO

IMG_0152
KIKOSI cha timu ya Young Africans kitashuka dimba la Uwanja wa Taifa siku ya jumapili kupambana na Wajelajela, Timu ya Jeshi la Magereza,Tanzania Prisons kutoka jijini Mbeya ikiwa ni mchezo wa pili wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara msimu wa 2014/2015.
Akiongea na tovuti rasmi ya klabu leo mara baada ya mazoezi, kocha mkuu wa Young Africans Mbrazil Marcio Maximo amesema vijana wake wako fiti kuelekea mchezo huo wa siku ya jumapili huku wakiwa wamejipanga kuhakikisha wanaondoka na pointi tatu muhimu.
Maximo amesema baada ya kupoteza mchezo wa awali dhidi ya wakata miwa wa Mtibwa Sugar, kikosi chake kimekua kikiendelea na mazoezi kila siku katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola huku wakiyafanyia marekebisho makosa yaliyojitokeza katika mchezo huo wa awali.
Kuhusu timu ya Tanzania Prisons, Mbrazil Maximo amesema anatambua walishinda mchezo wa awali dhidi ya Ruvu Shooting hivyo wana morali bado ya kuendeleza ushindi siku ya jumapili, lakini pia kikosi chake kipo fiti kusaka pointi tatu muhimu.
Aidha Maximo amesema habari njema kwa wana Yanga ni kurejea dimbani kwa kiungo Andrey Coutinho pamoja na mshambuliaji Jerson Tegete ambao wanatarajiwa kuonekana kwenye mchezo huo na kuhakikisha wanaisaidia timu yao kupata ushindi.
Wachezaji watakaoukosa mchezo wa siku ya jumapili ni Oscar Joshua na Hussein Javu ambao wote ni majeruhi, wakisumbuliwa na maumivu ya nyama za paja, na jumatatu wanatarajiwa kuanza mazoezi mepesi baada ya kuwa kwenye matibabu chini ya usimamizi wa daktari wa timu Dr Suphian Juma.
Marcio Maximo amewaomba wapenzi, washabiki, wanachama na wadau wa soka kwa ujumla kujitokeza kwa wingi siku ya jumapili katika mechi dhidi ya Prisons kuja kuwapa sapoti vijana na kuwashangilia muda wote wa mchezo.


Chanzo:shaffihdauda


RADIO ONE WAIBOMOA ZENJ FM: HUYU NDIO MTANGAZAJI WALIO MCHUKUA


Rama B akiwa na Kocha wa Simba Phiri

Kama  ukifika  Unguja  leo  hii  na ukimuuliza  hata  mtoto  mdogo  Rama  B  ni  nani  basi  jibu  utakalolipata  huyo  ni  mtangazi  mahiri  sana  wa  kipindi  cha michezo na burudani  cha  Zenji  fm, na kama  kuna  taarifa  iliyokuwa  gumzo kwa  wanamichezo  kwa  mwezi  ulipita  basi  ni  kuacha  kazi  kwa  ghafla  kwa  watangazaji  wawili  wa kutegemewa  wa  vituo viwili   ndugu  Itv  na  Radio  one  Maulid  Baraka  Kitenge  Maulid  Kambaya,siku chache  baada  ya  kuacha  kazi  Itv / Radio  One  watangazaji  hao  kila  mmoja  kwa  wakati  tofauti  aliripoitiwa  kujiunga  na  kituo  kipya  cha  redio  jijini  ambacho  kimekuwa  gumzo kwa  sasa cha  E  fm,hali  hiyo ilizua  hofu  kuwa  kipindi  cha  spoti  leo  huenda  kikadorora  na  hata  kupoteza  sifa  yake  tofauti  na awali  walivyokuwepo  Maulid  Kitenge   na  Katanga.
Kufatia  kuondoka  kwa  watangazji  hao  wawili  hali  ilionekana  kuwa  si  shwari  hasa  katika  kipindi  hicho  cha  spoti  leo   kuonekana  kama  hakina  mwenyewe  na  kuonekana  kama  kinakwenda  kwa kuunga  kuunga  hasa  pale  alipokuwa  hajulikani  ni  nani  sasa  mfanyaji  wa  kipindi  hicho  tofauti   na  awali, kuna  wakati  alisikika  Isac  Gamba, Deo Rweiyunga ,Amri  Masare  na mara  nyingine  pia  alisikika  Ally  Kashushu  ambaye  yeye  kwa  kawaida  huwa  anatangaza  michezo  kwenye  kituo  cha  redio  cha  Capital  fm  ambacho  pia  ni  kituo  chao.

USAJILI  WA  KIMYA  KIMYA.
Tofauti  na  kituo  kilicho  wanyakuwa  watangzaji  wao  kufanya  mbwe  mbwe  kwa  kuweka  picha  za  kuwasainisha  mikataba  watangazaji  hao  nyota  Redio  One  wao  wameonyesha  kukomaa   zaidi  kwa  kufanya  vitendo  kimya  kimya  kwani  mara  baada  ya  kufanya  usajili  wao  kimya  kimya  usio  na  mbwe  mbwe  hata  chembe  na tayari  sasa  ni  wiki  ya  tatu  tangu  wafanye  usajili  wao kwa  kumnyakua  mtangazaji  mahiri   kutoka  Kisiwani  Unguja  katika  kituo  kikubwa  sana  visiwani  humo  Ramadhan  Yusuf   Madogo  na  ameanza  kuunguruma   katika  vipindi  kadhaa  vya  Redio  One  kama  vile  Nipashe, Muziki  na  michezo na hata  kwenye  kipindi cha  leo  alisikika  samba samba  na  Amri  Masare,pia ameisha sikika  katika  kipindi  cha  Africa  Panorama na  Spoti  leo na  kuonyesha  kuwa  ana  uwezo  mkubwa   wa  kutangaza  na pia  wa  kuwenda  na  kasi  ya  kipindi  hicho.

RAMADHAN  YUSUF  MADOGO  NI  NANI?
Ramadhan  Yusuf  Madogo  ni  Kinyozi, Mwanamuziki  wa  muziki  wa kizazi  kipya, Mc  wa  shughuli  mbali  aliyegeukia  utangazaji, Ramadhan  Madogo  ni mtoto  wa  9  kati  watoto  14  wa  marehem  mzee  Yusuf  Madogo, alipata  elimu ya msingi  shule  ya  Kawawa  mkoani  Lindi na Elimu  ya  Sekondary  aliimalizia  katika  shule  maarufu  ya  High lands  ya  mkoani  Iringa  mwaka  1998,mwaka  1999  alifanya  kazi  ya kunyoa  kabla  ya  kuipa  kisogo  na kuingia  kwenye  muziki  wa kizazi  kipya kwa  takriban  miaka  8 na mpaka  leo  ana  nyimbo  zake  kadhaa  alizofanya  wakati  huo  ambapo  muziki  aliuanza  wakati  yupo  mkoani  Dodoma  wakati  akiishi  mkoani  humo, mwaka  2002 - 2003  aliachana  na  muziki  na kuingia  katika  chuo cha  Stone town  Computer, mwaka  2007  alijiunga  na  Zanzibar  Cable  Tv  akiwa  mtangazji  na  wakati  huo  alikuwa  akitangaza   vipindi  vya  sanaa  na  wasanii  tu,mwaka  2008  alijiunga  na  chuo  cha  cha  Royal   College  na   kufanikiwa  kupata  Diploma  ya  uandishi  wa  habari, na  baada  ya  mafunzo  hayo  ndiyo  akajiunga  na  Redio  ya  Chu chu  fm  ya  Marehemu  Yusuf  Chu  chu   Bwana  Chu  chu, mwaka  2009   alijiunga  rasmi  na  redio  ya  Zenji  fm  96.9  inayomilikiwa  na  Mh.Mohammed  Seif  Khatib  ana amedumu  nayo  kwa  miaka  takriban  6  mpaka  mwezi  huu  wa  September 2014 ndiyo  amejiunga  na  kituo  cha  Redio   One  huyu  ndiyo  Ramadhan  Madogo  al  maarufu  kama  RAMA   B  mtu   muhimu  sana  kwa  ZENJI  FM   wakati  huo, ambaye   wa Zanzbar  wanaona  ni  zaidi  ya  Kitenge  na  Katanga   kwa  kuwa  yeye  muandaaji  vipindi  mbali  mbali  siyo  michezo  pekee, alikuwa  akifanya  kazi  kwenye  vitengo  vyote  vya  Zenji  fm  kuanzia  Michezo, Vipindi  vya  Burudani, Vipindi  vya  habari  na  matukio na vya  kijamii  na  kisiasa  pia, Je  RAMA   B   ataweza  kuvivaa  viatu  vilivyovuliwa  na  Kitenge  na  Katanga ?


Friday, September 26, 2014

WASUSIA MASHINDANO KWA KUTAKIWA KUVUA HIJAB




Timu ya wanawake ya Qatar ya mchezo wa mpira wa vikapu imejiondoa kutoka mashindo ya bara Asia yanayofanyika huko Korea Kusini baada ya kuagizwa kuvua hijab kabla ya mechi yao dhidi ya timu ya Mongolia .

Wanawake hao walikataa kata kata kuvua vazi hilo na wakajiondoa mashindanoni wakidai inakiuka maagizo ya dina ya Kiislamu inayomtaka mwanamke kujistiri nywele zake haswa akiwa faraghani.

Sheria za shirika la mchezo huo duniani haziruhusu kuvaliwaj kwa vitambaa vya kichwani wakati wa mechi lakini sasa wamekuwa wakijadili iwapo sheria hiyo itaondolewe.

Hata hivyo ilipowadia wakati wa mechi yao dhidi ya Nepal sheria hiyo haikuwa imebadilishwa na hivyo iliwabidi kuyaaga mashindano. 

Fani nyengine za michezo katika mashindano hayo ya Bara Asia zinaruhusu uvaliwaji wa hijab.

Timu ya taifa ya unyanyuaji uzani ya Iran imekuwa ikishiriki mashindano hayo huku wakiwa wamevalia hijab.

Baraza la mashindano ya Olimpiki ya Bara asia OCA imesema kuwa haki za wachezaji ni zinapaswa kupewa kipaombele .


Baada ya kuyaaga mashindano hayo mchezaji wa Qatar Amal Mohamed A Mohamed alisema kuwa walikuwa wamehakikishiwa kuwa wataruhusiwa kushiriki mashindano hayo wakiwa wamevalia hijab na hivyo hawaelewi kwanini sheria hiyo haijabadailishwa.

''nina hakika kuwa hatutashiriki mashindano yeyote ya Bara Asia hadi sheria hiyo ibadilishwe''
Mashindano hayo hufanyika kila baada ya miaka 4 na huwaleta pamoja washiriki 9000 kutoka mataifa 45 yakishindana katika fani 36 ya michezo.

Mashindano hayo yatamalizika tarehe 4 Oktoba. 
Chanzo: BBC


Thursday, September 25, 2014

CHUO CHA IMTU CHAFUNGWA NA TCU

TUME ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) Imekifungia kwa mda,Chuo kikuu cha tiba na Sayansi IMTU kutofanya udahili kwa Wanafunzi wapya wa Mwaka wa Masomo 2014-2015,kutokana na chuo hicho kukiuka sheria ya inayosimamia Vyuo Vikuu nchini.

Uamuzi huo wa kikifungia Chuo hicho
Umetangazwa mda huu Jijini Dar Es Salaam na Kaimu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) Profesa Magishi N Mgasa wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari ambapo alisema maamuzi hayo yamefikiwa baada kikao cha Dharura kilichoitishwa na (TCU) wiki iliyopita na kujadili taarifa ya timu iliyotathimini chuo hicho, Ambapo kikao hicho kikabaini mapungufu makubwa katika chuo cha IMTU yakiwemo matatizo ya uongozi,kukosa wahadhiri wakutosha na wenye sifa,kutokuwepo na Vifaa pamoja na kudahili wanafunzi bila hata kuwa na taratibu zilizowekwa na tume.

Profesa Mgasa alisema kwa kufanya hivyo chuo cha IMTU imekiuka sheria ya namba 5(1),sura ya 346 ya sheria za Tanzania ambayo inakitaka chuo Kikuu chochote kufuata taratibu zilizowekwa na tume.
Vilevile Profesa Mgasa alizidi kusema baada ya Tume kubaini makosa hayo,ndipo wamefikia maamuzi ya kukifungia chuo cha IMTU kufanya
udahili kwa wanafunzi wapya wa Mwaka
2014-2015,mpaka pale itakakapo rekebisha mapungufu yaliyotajwa na Tcu.

Pia tume imetoa notsi ya miezi 3 kwa chuo cha IMTU,kuanzia tarehe 16 mwezi huu kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza na endapo chuo hicho kikikaidi basi TCU haitosita kuwachukulia hatua kali ikewemo hata kukifungia kabisa.
Aidha Profesa Mgasa aliwataka wanafunzi nchini wasijiunge na chuo Kikuu chochote bila ya kufuata maelekezo kutoka Tume ya vyuo Vikuu
nchini (TCU).


DOWNLOAD RASIMU YA KATIBA MPYA INAYOPENDEKEZWA NA BUNGE MAAALUM

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta

 Mambo yameiva, na hii hapa ndiyo Rasimu ya Tatu ya Katiba, ambayo inapendekezwa na Bunge Maalum. 

Vipengele vingi vimebadilishwa. Haya hapa ni mambo ya Muungano:

Mambo ya Muungano
 
1. Katiba na Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

2. Ulinzi na usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

3. Usalama na usafiri wa anga.

4. Uraia na uhamiaji.

5. Jeshi la Polisi.
 

6. Sarafu na Benki Kuu.

7. Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na Mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini Tanzania na zinazosimamiwa na Idara ya Forodha.

8. Mambo ya nje.

9. Usajili wa vyama vya siasa.

10. Mahakama ya Juu na Mahakama ya Rufani.

11. Elimu ya Juu.

12. Baraza la Taifa la Mitihani na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza hilo.

13. Utabiri wa hali ya hewa.
 

14. Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano. 
 

DOWNLOAD/IPAKUE MWENYEWE HAPA: RASIMU YA TATU

DEREVA TAX NA MWANDISHI WA HABARI WALISAIDIA NYERERE ASIPINDULIWE

SIRI ya mashujaa waliozima jaribio la kutaka kupindua Serikali ya Tanzania chini ya Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1982, imewekwa hadharani kwamba mashujaa hao walikuwa vijana wawili; mmoja dereva wa teksi na mwingine mwandishi wa habari wa gazeti la Serikali la Daily News.

Akitoboa siri hiyo katika Maadhimisho ya Siku ya Amani Duniani, aliyekuwa Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Balozi Augustine Mahiga, alisema kama si vijana hao, huenda mapinduzi yangefanyika na yangefanikiwa, amani ya Tanzania leo isingekuwepo.

Akisimulia ilivyokuwa, Balozi Mahiga ambaye alikuwa Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa akiwa kijana wa miaka 30, alisema kuna kijana wa miaka 23 aliyekuwa dereva wa teksi (bila kumtaja jina), ambaye alipata taarifa hizo ambazo Serikali haikuwa nazo.

Baada ya kupata taarifa hizo, Balozi Mahiga alisema kijana huyo alimweleza mwandishi wa
habari wa Daily News (bila kumtaja jina), ambaye naye alikuwa kijana mdogo wa miaka 27, ambaye alipeleka taarifa hizo kwake.

Kwa mujibu wa Balozi Mahiga, alipopata taarifa hizo, aliamua kufanya uchunguzi na kubaini kama kweli kulikuwa na mpango wa kutaka kupindua Serikali, ambao waliuzima kwa kukamata washukiwa ambao walipelekwa mahakamani na kufungwa.

Watu hao ambao alisema walisamehewa wakati wa uongozi wa Awamu ya Pili, sasa wapo huru lakini mpango wao kama ungefanikiwa, huenda amani iliyopo sasa isingekuwepo kwa kuwa kuipoteza ni rahisi kuliko kuirejesha.

“Rasilimali kubwa ya amani ni vijana kwa kuwa kama si wale vijana kutoa taarifa, mapinduzi yangetokea na amani iliyopo sasa isingetokea…amani ikipotea ni shida kuirejesha.

“Msiombe kutokee vita…mimi nimeona watu wanaoishi katika vita, hawana hata muda wa kula wala kulala, akifa mmoja mwingine anabeba silaha anaendelea,” alisema Balozi Mahiga.
Daily News ni moja ya magazeti yanayochapishwa na Kampuni ya Magazeti ya Serikali ya TSN, mengine yakiwa HABARILEO, HABARILEO Jumapili, Sunday News na SpotiLEO.

HabariLeo: Mwandishi TSN atajwa kuzima uasi


WANAFUNZI WALIO CHAGULIWA KUJIUNGA NA VYUO VIKUU MBALIMBALI TANZANIA


Nakala hizi ni zimepatikana via JamiiForums


SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 25 SEPTEMBA HAPA




MAN CITY YAIRARUA SHEFF WEDNESDAY

Timu ya Man city usiku wa kuamkia leo imeishushia kipigo kikubwa cha mabao timu changa ya Sheff Wed kwa kuitandika 7 kwa 0, Mabao hayo yaliwekwa kimiani na Lampard dk ya 47 na 90, Dzeko 53 na 77, Jesus Navas dk ya 54, Yaya Toure dk ya 60 kwa penati.
Dzeko akiukwamisha wavuni mpira kama anavyoonekana hapo akiwa ameruka juu.
Frank Lampard akishangilia kwa kugongeana na Navas katika moja ya bao lake.
 Makocha wa timu zote mbili katika harakati zao uwanjani hapo.




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU