Kwa mujibu wa Page ya mwandishi maarufu wa habari za michezo ndugu Edo Kumwembe amesema kuwa Mrisho Khalfan Ngassa amehalalishwa kuchezea Yanga na atarudisha hela asilimia hamsini ya gharama za Simba na amefungiwa mechi sita.
Hapo chini ni jinsi Bwana Edo Kumwembe alivyo andika:
CHINI NI HABARI HIYO KUTOKA VYANZO VINGINE:
  
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imepitia usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom na kumuidhinisha Mrisho Ngasa kuchezea timu ya Yanga baada ya kukamilisha usajili wake.
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imepitia usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom na kumuidhinisha Mrisho Ngasa kuchezea timu ya Yanga baada ya kukamilisha usajili wake.
Hata
 hivyo, Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa imebaini 
kuwa Ngasa alisaini mkataba mwingine Simba (katika kipindi ambacho 
alikuwa na mkataba na Azam) ambapo anatakiwa kurejesha fedha alizopokea 
(sh. milioni 30) pamoja na fidia ya asilimia 50 (sh. milioni 15) ya 
fedha hizo kwa Simba.
Kamati
 pia imemfungia mechi sita za mashindano (kuanzia mechi ya Ngao ya 
Jamii), na anatakiwa awe amelipa fedha hizo ndani ya kipindi hicho cha 
kukosa mechi hizo. Akishindwa, hataruhusiwa kucheza hadi atakapolipa 
fedha hizo.
Vilevile
 Kamati imepitia pingamizi zote zilizowasilishwa kuhusu usajili wa 
wachezaji, kukatiza mikataba ya wachezaji na kuzitaka klabu husika ziwe 
zimetatua masuala hayo hadi Alhamisi (Agosti 22 mwaka huu).
Kwa
 upande wa wachezaji wa kigeni, Kamati imeagiza wasiruhusiwe kucheza 
hadi watakapopata Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC) pamoja na vibali 
vya kufanya kazi nchini (work permits).
Kamati
 hiyo itakutana tena Ijumaa (Agosti 23 mwaka huu) ili kupata ripoti za 
pingamizi ilizoagiza ziwe zimefanyiwa kazi hadi Agosti 22 mwaka huu na 
kutoa uamuzi kwa pande ambazo hazikuafikiana.
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
